Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wachina wanyang'anywa ujenzi barabara Singida
Wachina wanyang'anywa ujenzi barabara Singida
By Habari Tanzania | Published  02/14/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Mwandishi Wetu, Singida

SERIKALI imeinyang'anya Kampuni ya Sietco eneo la urefu wa kiliomita 30 mkoani Singida na kuipatia Kampuni ya Konoike, baada ya kubainika kuwa kampuni hiyo haina uwezo wa kuijenga kutokana na kuwa na vifaa chakavu.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Perseko Kone, alisema jana kuwa ni kweli Sietco wameshindwa kukarabati sehemu korofi za eneo la Mkiwa, Isuna na Kamenyanga.

Kone alisema kutokana na hali hiyo, serikali imeamua kuingia mkataba mpya na Kampuni ya Konoike wa kujenga kilomita 30 kutoka Manyoni hadi Mkiwa kupitia Kamenyanga na Sietco imebakiwa kilomita 25 za kutoka Isuna hadi Mkiwa.

Siteco iliyopewa zabuni ya kujenga barabara ya Singida Manyoni, imeshindwa kabisa kurekebisha sehemu korofi zilizo haribika vibaya kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha na kusababisha magari kukwama kwa zaidi ya siku nne.

Kone alisema hadi kufika Jumatano wiki, iliyopita, Kampuni ya Konoike ilikuwa imekwisha kuanza kutengeneza maeneo yaliyo kuwa yameharibika, ikiwamo eneo la Kamenyanga ambako magari yalikuwa hayapiti kabisa kutokana na kuharibika kwa barabara.

Kone alisema serikali kupitia wakala wa barabara (Tanroads) mkoani Singida
imeweka mkakati wa kuhakikisha kuwa uzembe wa kampuni za ujenzi unadhibitiwa kwa kufuatilia kwa makini matengenezo ya barabara.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Lawrencre Tarimo, alisema hali ya barabara katika maeneo hayo sasa ni nzuri kwani magari yameanza kupita.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.