Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Yatangaza ajira 9,000 kwa walimu
Yatangaza ajira 9,000 kwa walimu
By Habari Tanzania | Published  02/9/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated

SERIKALI inatafuta walimu zaidi ya 9,000 wanaotakiwa kufundisha katika sekondari mpya zilizofunguliwa na wananchi, kabla ya Machi mwaka huu.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Margaret Sitta alisema jana kuwa Wizara inataka walimu hao kutokana na idadi ya wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwanza mwaka huu kuongezeka na kufikia asilimia 90 badala ya asilimia 75.

Vijana waliomaliza kidato cha sita na kufaulu wametakiwa kuomba nafasi hizo na watapewa mafunzo ya mwezi mmoja katika vyuo mbalimbali vya ualimu nchini, alisema. Alisema wanahitajika vijana 6,000 kuhudhuria mafunzo hayo kwenye vyuo vya Monduli, Morogoro, Korogwe, Mpwapwa, Tabora, Tukuyu, Butimba, Mtwara na Kleruu. Waziri alishauri vijana hao waombe nafasi katika vyuo vilivyo karibu na mikoa yao.

Mafunzo hayo yataanza Februari 26 na yatamalizika Machi 24 na wote watakaomaliza watasambazwa katika sekondari mbalimbali kwa ajili ya kufundisha, alisema. Kuhusu walimu wengine, Waziri alisema walimu wengine 3,124 watakaomaliza mitihani ya stashahada mwezi huu nao watapangiwa katika shule mbalimbali kupunguza upungufu huo.

Wizara pia itaajiri walimu 450 kutoka vyuo vikuu na walimu wastaafu 250 wataajiriwa kwa mkataba alisema na kuongeza kuwa idadi ya walimu wote wanaohitajika ni 9671 ambao watatawanywa katika shule mpya 667 za sekondari zilizofunguliwa mwaka huu.

Alisema serikali imetenga fedha kwa ajili ya kugharamia mafunzo ya muda mfupi ya walimu watakaohudhuria mafunzo ya mwezi mmoja na watalipwa mishahara yao watakapoanza kazi kwa sababu iko tayari.

Waziri alisisitiza kuwa vijana wanaotaka kujiunga na mafunzo hayo ni lazima wapeleke maombi yao kabla ya Februari 15 ili yaweze kufanyiwa kazi haraka na waanze masomo yao.

Akizungumzia wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwanza alisema kati ya wanafunzi 467,997 waliofaulu mwaka huu kujiunga na kidato cha kwanza, wanafunzi 421,368 watajiunga na sekondari baada ya shule hizo kuongezeka. “Wananchi wameonyesha moyo wa kujenga sekondari, ni jukumu letu kutafuta walimu ili wakafundishe kwenye shule hizo,” alisema.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.