Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Ramadhan Semtawa  »  Makampuni ya kigeni yajitosa kukarabati kivuko
Makampuni ya kigeni yajitosa kukarabati kivuko
By Ramadhan Semtawa | Published  02/8/2007 | Ramadhan Semtawa | Unrated

Na Ramadhan Semtawa

MAKAMPUNI matatu ya kigeni, yamejitosa kutaka kukifanyia matengeneza kivuko cha Mv Kigamboni ambacho kiko katika hali mbaya.

Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Ufundi na Umeme kutoka Wizara ya Miundombinu, John Ndunguru, aliyataja makampuni hayo kuwa ni Ms Johs Gram-Hanseen ( kutoka Denmark), Ms Dutchmed International B.V (Uholanzi) na Ms Neue Ruhr Stert Schiffsweft (Ujerumani).

Alisema makampuni hayo na la Ms Professional Marine Contractors LTD la hapa nchini, yaliyoomba zabuni hiyo baada ya kufunguliwa wiki iliyopita.

Ndunguru, alisema kinachofanyika kwa sasa ni kupitia zabuni hizo na kuona kampuni iliyokidhi vigezo vya kutengeneza kivuko hicho.

" Makampuni yaliyoomba ni manne, matatu ya kigeni, tayari zabuni imekwishafunguliwa, kinachofanyika sasa ni tathimini," alifafanua.

Kivuko cha Mv Kigamboni kinataka kufanyiwa matengenezo makubwa ambayo yatakifanya kusimama kazi kwa kipindi cha miaka miwili.

Tayari Wizara ya Miundombinu kupitia kitengo hicho cha umeme, kimetangaza zabuni ya kutafuta kivuko cha kukodi ambacho kitachukua nafasi ya Mv Kigamboni.

Moja ya vigezo ya kivuko hicho ni kutaka kiwe na uwezo wa kubeba abiria hadi 800 kwa wakati mmoja.

Mv Kigamboni kiko katika hali mbaya na mara kwa mara kimekuwa kikizima baharini na wakati mwingine kupoteza mwelekeo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Nthelezi Nesaa
  4. Linda Garner
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.