Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mabomu yaliyolipuka Dar yalitoka Tabora
Mabomu yaliyolipuka Dar yalitoka Tabora
By Habari Tanzania | Published  02/8/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Simon Berege, Dodoma

WATAALAM wa Kikosi cha Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) cha 302, wamegundua kwamba baadhi ya wananchi wakijipenyeza kwa siri kwenye uwanja wa shabaha wa Shule ya Mafunzo ya Kijeshi ya Kalunde, mkoani Tabora na kukusanya mabomu yaliyochwa kwenye eneo hilo wakidhani ni vyuma chakavu.

Akiwasilisha taarifa ya hali ya uhalifu nchini bungeni jana, Waziri wa Usalama wa Raia, Bakari Mwapachu, alisema wachunguzi hao waliwahoji watu 14 na kubaini kwamba mizigo mingi ya chuma chakavu iliyogundulika kuwa na mabomu, ilitoka mkoani Tabora, hivyo walienda kufanya ukaguzi.

Alisema baada ya kupata mabomu hayo, uchunguzi umeonesha kwamba watu hao huyakusanya na kuyajumuisha na vyuma vingine chakavu, kisha kuvisafirisha
kwenda Dar es Salaam kwa wenye viwanda vya nondo ambako wahusika hushindwa kuyatambua mabomu hayo.

Uchunguzi huo unafuatia tukio la kulipuka kwa bomu moja katika eneo kiwanda cha nondo kilichoko wilayani Temeke, jijini Dar es Salaam Desemba 27, mwaka jana

Alisema ili kukabiliana na hali hiyo isitokee tena, Serikali iliunda timu iliyoshirikisha wajumbe kutoka jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa , JWTZ , Mkemia
Mkuu wa Serikali, kuchunguza vyanzo vya mabomu na kushauri hatua za kuchukua ili tukio kama hilo lisitokee tena.

Mwapachu alisema kwamba hadi kufikia Januari mwaka huu, jeshi lilikwisha kagua
maeneo ya viwanda saba vinavyotengeneza nondo jijini Dar es Salaam.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.