Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  EAC wamuenzi Julius K. Nyerere
EAC wamuenzi Julius K. Nyerere
By Habari Tanzania | Published  02/8/2007 | Habari za Kitaifa | Rating:
Na Claud Gwandu, Arusha

JUMUIYA ya Afrika Mashariki (EAC), itaanzisha kituo cha utafiti wa amani na utatuzi wa migogoro katika nchi za Kusini mwa Afrika.

Kituo hicho ambacho kitakuwa na ofisi kwenye makao makuu ya jumuiya hiyo mjini Arusha, kitaitwa Nyerere Peace Research Centre, kwa heshima ya Baba wa Taifa, Marehemu Mwalimu Julius Nyerere.

Kwa mujibu wa Msemaji wa EAC, Magaga Alot, uamuzi wa kuanzishwa kwa kituo hicho, ulifikiwa Februari 1, mwaka huu katika kikao cha Baraza la Mawaziri wa Jumuiya hiyo, kilichofanyika mjini hapa.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana, A lot, alisema kituo hicho kitashirikiana na Chuo Kikuu cha Arcadia cha Marekani katika shughuli za utafiti wa migogoro na usuluhishi.

Mkataba wa ushirikiano huo katika ya EAC na Chuo kikuu hicho, ulitiwa saini mwishoni mwa wiki iliyopita, katika makao makuu ya jumuiya hiyo.

Malengo ya kituo hicho, ni pamoja na kufanya utafiti kuhusiana na migogoro katika nchi za Afrika na kuwapa watunga sera serikalini, matokeo ya utafiti huo kwa ajili ya utekelezaji.

Kituo hciho kimepewa jina la Nyerere ikiwa ni kutambua na kuenzi mchango wake katika kutetea ukombozi wa nchi za Afrika na pia kazi za usuluhishi alizokuwa akizifanya wakati wa uhai wake katika nchi zenye migogoro kama Burundi.

Kabla ya kifo chake, Oktoba 14, mwaka 1999 kilichotokea katika hospitali ya Mtakatifu Thomas nchini Uingereza, Nyerere alikuwa Mwenyekiti wa Mazungumzo ya kutafuta Amani nchini Burundi, kati ya serikali ya nchi hiyo na waasi.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.