MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete, mkoani Iringa, Onna Nkwama amefikishwa mahakamani akituhumiwa kuzini na mke wa mtu.
Nkwama ambaye hata hivyo hakuweza kufika mahakamani jana amefunguliwa kesi hiyo na Ephraim Cheyo, Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wilayani Makete. Katika kesi hiyo Cheyo anamtaka Mwenyekiti huyo kumlipa fidia ambayo hata hivyo haikuwekwa wazi.
Kesi hiyo ilitajwa jana mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa, Sekela Mwaiseje. Hata hivyo wakili anayemtetea mlalamikaji, Justin Mshokorwa na wakili wa upande wa utetezi, Basil Mkwata kwa pamoja waliiomba mahakama kuipeleka kesi hiyo katika baraza la usuluhishi la mahakama iweze kupatiwa ufumbuzi.