Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mbolea ya ruzuku yayeyuka Kahama
Mbolea ya ruzuku yayeyuka Kahama
By Habari Tanzania | Published  02/5/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Alli Lityawi

MKUU wa Wilaya ya Kahama, Kanali Kelvin Msemwa, amesema utaratibu mbovu uliowekwa na wakala walioteuliwa na halmashauri, ndio kikwazo cha mbolea ya ruzuku kuwafikia wakulima.

Akizungumza juzi katika kikao cha Baraza la Madiwani baada ya kubainika kuwa pembejeo hiyo muhimu haikuwafikia wakulima, Msemwa alisema ugawaji wa mbolea ya ruzuku kupitia mawakala unafanywa kibiashara zaidi.

“Nina shaka na utaratibu huo uliotumika wa kuchanganya huduma na biashara, ni lazima mkulima anyanyasike, ni muhimu tubuni utaratibu mbadala,” alishauri.

Awali, madiwani wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Kahama (CCM), James Lembeli, walidai mbolea hiyo haikuwafikia walengwa kama ilivyopangwa.

Mbolea nyingi ya ruzuku inafikishwa vijijini na walanguzi ambao wanawauzia wakulima kwa sh 40,000 kwa mfuko mmoja badala ya sh 23,000.

Hata hivyo, pamoja na madai hayo, wataalamu wa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Kahama, walikiambia kikao hicho kuwa, tayari wameishasambaza tani 100.5 katika kata ambazo zilithibitika zina wakulima wa tumbaku, ambao hukopeshwa pembejeo za kilimo na kampuni za tumbaku kupitia vyama vyao vya msingi.

Aidha, baada ya kubanwa na madiwani, Ofisa Kilimo na Mifugo, Isaya Ndaga, alikiri kuwa mawakala waliopewa kazi hiyo wamekuwa wakiuza mbolea hiyo nje ya utaratibu na kisha kutoa takwimu za uongo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.