Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Chuo kikuu Dar huenda kikakopesha wanafunzi wake
Chuo kikuu Dar huenda kikakopesha wanafunzi wake
By Habari Tanzania | Published  02/1/2007 | Habari za Kitaifa | Rating:

Na Kizitto Noya

UONGOZI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), unadaiwa kuwa unaangalia uwezekano wa kukopesha wanafunzi wake asilimia 40 ya gharama zote za masomo wanazotakiwa kulipa kwa ajili ya masomo.

Hatua hiyo imekuja baada ya wanafunzi wa vyuo vikuu jijini Dar es Salaam, kuandamana kupinga agizo la Serikali linalowataka wachangie gharama za masomo kwa kiwango hicho.

Habari zilizopatikana chuoni hapo juzi zinadai UDSM kinaangalia uwezekano wa kuwakopesha wanafunzi wake kiasi hicho, ambacho watatakiwa kukirudisha kabla au baada ya kumaliza masomo.

Inadaiwa kuwa, uongozi wa chuo hicho, umekubali kuangalia uwezekano wa kutowadai wanafunzi wake gharama hizo, baada ya kupokea maombi kutoka kwa uongozi wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu Dar es Salaam (DARUSO).

Rais wa DARUSO, Magesa Mwita, alisema suala la chuo kuwadhamini wanafunzi hao kwa asilimia 40 wanayotakiwa kuchangia, bado lipo kwenye mjadala na linahitaji baraka za Baraza la Chuo litakalokutana mwezi ujao.

Afisa Uhusiano Mkuu wa Chuo hicho, Julius Saule, alikataa kuzungumzia chochote kuhusiana na suala hilo kwa madai kuwa sio wakati muafaka.

Alisema madai ya wanachuo kutaka wasichangie gharama za masomo ni ya muda mrefu na tayari serikali imeshatoa uamuzi, hivyo sio busara chuo kuzungumza chochote sasa mpaka hapo itakapopatia ufumbuzi suala hilo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by James)
    Rating
    That will be a good idia, because most of the students are from poor families, as we know the status of our economy in villges.
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.