Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Kamati ya Wangwe yakimbia Zanzibar
Kamati ya Wangwe yakimbia Zanzibar
By Habari Tanzania | Published  01/31/2007 | Habari za Kitaifa | Rating:

Na Salma Said, Zanzibar

KAMATI ya kukusanya maoni ya Uharakishaji wa Kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki imekatisha muda wake visiwani Zanzibar, kwa madai kuwa muda waliopanga hautoshi na wananchi wameonekana hawaelewi kinachotakiwa kufanyika

Kutokana na sababu hizo zilizotolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Profesa Samwel Wangwe, kamati hiyo imetumai siku mbili tu badala ya siku tano zilizokuwa zimepangwa.

Alisema kamati hiyo haikutarajia kukuta uelewa wa wananchi katika visiwa hivyo kuhusiana na Shirikisho la Afrika Mashariki kuwa chini namna hiyo, hivyo aliwataka waendelea kujifunza na kupata ufahamu zaidi ili kamati hiyo itakaporudia baadaye waweze kuchangia vizuri zaidi.

Profesa Wangwe alisema shughuli za ukusanyaji wa maoni Zanzibar zilisitishwa kuanzia jana.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo alisema kamati yake itazidi kutoa elimu ya kuwahamasisha wananchi mbalimbali kutumia fursa hiyo kutoa maoni na alitoa wito kwa wananchi wa Zanzibar kujiandaa kutoa maoni hapo baadaye kamati hiyo itakaporudi tena visiwani katika kipindi cha mwezi Aprili na Mei.

Kamati hiyo imetoa uamuzi huo, ikiwa tayari imekusanya maoni ya baadhi ya wananchi na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliotoa maoni kwa kamati hiyo na kuonyesha wasiwasi wa Zanzibar kumezwa katika Shirikisho hilo.

Wengi wao, bila kujali itikadi zao za kisiasa, waliungana kupinga shirikisho hilo na kushauri kwamba kama ni lazima Tanzania kujiunga basi ni vyema Zanzibar ikajiunga kama Taifa linalojitemegea.

Miongoni mwa watu wazito waliolizungumzia shirikishi hilo, ni Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, ambaye alisema Zanzibar bado inakabiliwa na matatizo mengi ikiwemo lile la mgogoro wa kisiasa na kero za muungano hivyo ni vyema mambo hayo yakatafutiwa ufumbuzi kwanza kabla ya kujiunga na shirikisho la Afrika Mashariki.

Kificho aliyasema hayo jana wakati wa kutoa maoni juu ya kuanzishwa kwa shirikisho la Afrika Mashariki katika ukumbi wa baraza la wawakilishi jana mjini hapa.

Alisema ni jambo zuri kujiunga na shirikisho, lakini ni mapema na kwa Zanzibar inayokabiliwa na mambo mengi hivi sasa.

Alisema kutokana na michango ya wajumbe wengi waliochangia inaonesha dhahiri kwamba hawakatai shirikisho moja kwa moja lakini walichoogopa ni wakati huu, kwa vile ni mapema mno nchi kama Tanzania kujiunga na umoja huo.

Kamati hiyo itandelea na kukusanya maoni ya Watanzania kwa upande wa Mikoa ya Tanzania Bara. Hadi sasa ni wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam ndio waliokwisha toa maoni yao.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by zinduka)
    Rating
    Waliosema kuwa usishangae ya Musa utayaona ya firahuni hawakukosea kabisa. Wangwe na kamati yako mnakimbia nini Zbar?????
    Wananchi wenye taaluma mbalimbali walikwisha sema siku nyingi kuwa kabla ya mchakato wa kutoa maoni kwa Wangwe kuhusu EAF, wananchi walitakiwa kwanza kuelimishwa juu ya nini faida ya hili shirikisho, na lina tofauti gani na lile lililovunjika 1977.
    Uundwaji wa hili shirikisho umejaa zaidi usanii na siasa. Sasa kama wenye nchi wameshaamua kufanya walitakalo, basi walifanye tu kwa raha zao. Wala wasitake kufanya watanzania hawana akili ya kujua nini kizuri na nini kibaya kwao.
    Hayo mamilioni ya pesa yaliyotengwa kwaajili ya kukusanya maoni, toka kwa waTZ kuhusu shirikisho wasilolijua, ingekuwa bora yakatumika katika kutoa elimu nchi nzima kuhusu EAF, kuliko yanavyotumika hivi sasa. Wananchi tumechoka kufanywa kama tupo usingizini!!!!!! Ukweli nikuwa wananchi tupo macho, tena tupo macho sana. That's for sure.
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.