                
|
|
| BBC yaidhalilisha Tanzania Uingereza |
| By Habari Tanzania |
Published
06/15/2006
|
Habari za Kitaifa
|
Unrated
|
|
|
|
Na Said Mohamed, London
WAKATI Serikali ya awamu ya nne imekamia kuitangaza Tanzania nje, Jumanne iliyopita televisheni ya BBC juzi imeonesha program maalum yenye kuelezea maovu na vitendo vya udhalilishwaji wa binadamu vinavyofanywa nchi Tanzania. Kipindi hicho kilichorushwa kwa saa moja na nusu kuanzia saa sita usiku hadi saa saba na nusu, kilionesha jinsi mazingira machafu ya utengenezaji wa minofu ya samaki na watoto wadogo wanavyofanyiashwa kazi mjini Mwanza, Tanzania. Pia katika program hiyo imeonesha jinsi wanawake wanavyojiuza mjini Mwanza, kuwahoji wagonjwa wa ukimwi na uwanja wa ndege wa Mwanza unavyotumika kuleta silaha ambazo nyingi zinatumika kwa nchi jirani kwa kuwa hauna ulinzi imara. Kipindi hicho ambacho juzi kilikuwa gumzo kubwa hapa London kwa Watanzania wanaioshi na kufanya kazi hapa, kimeiweka jina zuri la Tanzania gizani kutokana na kuoneshwa sehemu kubwa ya maovu na mabaya na hakukuwa hata moja zuri katika muda wa saa moja na nusu ya prpgram hiyo. Mtayarishaji wa kipindi hicho alionesha jinsi samaki aina ya sangara wanavyovuliwa na kwenda kuchuna minofu na baada ya hapo vinchwa vya samaki hao vinapelekwa sehemu nyingine ambayo kinamama wanavianika, Lakini mpiga picha huyo aliweza kuonesha vichwa hivyo vya sangara vinavyotoa funza kutokana na mvua zilizokuwa zinanyesha, pia walionesha jinsi watoto wadogo wanavyofanya vibarua katika pwani ya ziwa Victoria, hali ambayo mtangazaji alidai ni ukiukwaji wa haki za binadamu. Katika programu hiyo ya BBC, pia walionesha jinsi uwanja wa mdege wa Mwanza husivyokuwa na ulinzi na hivyo kila ndege inatua hapo hata kama haifanyi kazi ya kuchukua samaki, hali aliyaodai kuwa muda mwingine ndege nyingine zinaleta siraha au madawa ya kulevya. Baadhi ya Watanzania walihojiwa na mwandishi wa habari hizi kuhusu kipindi hicho ambacho kinadaiwa kimekuwa kikirushwa mara kwa mara katika televisheni hiyo, wamesikitishwa kwa jinsi filamu hiyo inavyoielezea Tanzania na lengo lilikuwa ni kuichafua jina zuri la nchi. Alipotafutwa juzi, balozi wa Tanzania hapa Uingereza, Haassan Kibelloh ili kujua msiimamo wa Serikali kuhusu programu hiyo inayooneshwa mara kwa mara katika BBC, inadaiwa hakuwepo hapa na badala yake yupo Tanzania kwa shughuli nyingine za kikazi. Lakini afisa mmoja wa ubolozi huo, ambae hakupenda jina lake litajwe alisema walishapata taarifa hizo na baadhi yao kukiona kipindi hicho na kuahidi Serikali inalifahamu hilo na inalifanyika kazi kwa kasi na nguvu na tayari kulikuwa na kikao cha maofisia kuhusu hiyo programu. Bw. Ahemd Ali, Mtanzania anaehishi London alisema lengo la BBC ilikuwa labda kushindana na televisheni ya Sky inayoonesha kipiondi cha Tanzania Vision chenye kuelezea mazuri ya Tanzania, hivyo wanataka kuonesha wao wanavyoijua Tanzania. “Sky wamekuwa wakionesha kipindi cha Tanzania kila Ijumaa, ambapo tumekuwa tukionea mengi kuhusu nchi yetu ambayo kweli inavutia watu wengi, sasa hao naona wanataka kupingana na hilo, “ alisema Bw. Ali. Hata hivyo juhudi za kuwatafuta waandaji wa kipindi cha Tanzania Vision chenye lengo la kuitangaza Tanzania hapa Ulaya, Bw. Juma Pinto na Bw. Abuu Faraji kuhusu maoni yao kuhusu kipindi hicho, hawakuweza kupatikana na mmoja wa maofisa katika ofisi yao walidai kuwa wapo Ujerumani kwenye fainali ya kombe la Dunia. Mfanyabiashara maarufu, Emanuel Sindi anayefanya biashara na wenzake wa Uingereza alioenakana kusononekana na hiyo program na kudai kuwa inaondoa uaminifu mkubwa kwa nchi yetu na kufikilia sehemu kubwa ya Tanzania ndivyo inavyoonekana au mazingira yote ndicyo yalivyo. "Sisi wafanyabishara tumejenga heshima kubwa na inaonyesha namna wafanyabiashara wa Tanzania wanavyoweza kujenga uaminifu na heshima katika mashirikisho ya kimataifa na hii pia ni heshima kwa Rais Jakaya Kikwete, lakini vipindi kama hivi vinatuondolea heshma yetu katika mataifa ya nje,” alisema. Bw.Sindi alisema amekuwa akingalia kipindi cha Tanzania Vision mara kwa mara, kimekuwa kikielezea mambo mazuri ya Tanzania, tunaona mlima Kilimanjaro, jinsi viwanfda vyetu vinavyofanya kazi, hutuba za Rais Kikwete, sasa hawa BBC wanaonesha vitu gain hivi? Profesa Harun Kundi yeye alisema kuwa Serikali haina budi kuchukua hatua za hara kukikomemsha programu hiyo kurushwa tena katika teelevisheni ya BBC, la sivyo heshama ya nchi yetu na sisi Watanzania itapungua huku Ulaya “Hiki kipindi kimewauma watu wengi sana, mimi sikutaka hata kuendelea kuangalia kwani ni mambo ambayo hayakufaha kuoneshwa na hata hizo picha zilivyokuwa vinapigwa inaonekana mpigaji alikuwa anaiba tena kwa kujificha, sasa hii si sheria,” alisema Bw. Kundi kwa masikitiko. Serikali ya awamu ya nne inafanya jitihada za makusudi kuhakikisha kuwa Tanzania inajitangaza nje kwa lengo la kuvutia watalii na wawekezaji na hivi karibuni Waziri Mkuu, Edward Lowassa alipokuwa njiani kwenda Marekani alipata nafasi ya kukutana na viongozi wa kampuni ya Jambo hapa London na kuwaomba kuongeza juhudi zao katika kuitangaza nchi.
|
Comments
-
Comment #1
(Posted by Maxence M. Melo)
Unrated
Huku si kudhalilisha bali kuonyesha UHALISIA wa mambo. Inatakiwa tuache UNAFIKI na kuongea UKWELI wa mambo ili wahusika WABADILIKE. Kulindiana majina inakuwa ni kuharibu. Hapa naamini UJUMBE UMEFIKA kwa wahisika!
Mungu Ibariki Tanzania
-
Comment #2
(Posted by Mussa)
Unrated
Mimi ningependa kuuliza wale wanaosema kwamba Tanzania ilidhalilishwa.Lipi katika kipindi hicho lilikuwa si la kweli?
-
Comment #3
(Posted by an unknown user)
Unrated
Ukweli ni kitu bora, Wanasiasa hawependi ukweli wanapenda kudanganya wenzao tu. haya kasi mpya fagia uozo. Tanzania tutangazwe nje kwa ukweli na sio kiini macho. Suala la silaha kongo ni la kweli kabisa na samaki ni kweli.
-
Comment #4
(Posted by shaul)
Unrated
watanzania msilalamike huo ni ukweli mtupu hakuna la uwongo wala kudhalilishwa labda huyo mtayarishaji atasaidia sasa tanzania kubadilika ili iweze kusifiwa.msiwe manaficha maovu mi nimefurahi sana waendelee hivyo hivyo mbona india hawalalamiki mnadhani hawaoneshwi?RAIS BADILISHA HIYO HALI SIO KULALAMIKA KAMA HAMNA AKILI VILE
-
Comment #5
(Posted by Bernard)
Unrated
Wabongo bwana!!!! mkiambiwa ukweli inakuwa nongwa. Haya sasa semeni. Je waneonyesha jinsi kinyesi kinavyotapishwa ndani ya ziwa kutokea milima ya Bugando ???!!!!!
-
Comment #6
(Posted by Mtanzania)
Unrated
Tukumbuke usemi unaosema'NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO'.Kama kuna kilicho cha uongo ambacho jamaa wa BBC walikisema basi tunaweza kulalamika, lasivyo TUBADILIKE.
Ukweli unauma sanaaana!!
-
Comment #7
(Posted by an unknown user)
Unrated
Mambo ya siraha tumeanza kuyasikia si leo. Hata katika magazeti yetu hapa nyumbani yamekwisha andikwa hapo nyuma.
Masuala ya samaki, yameanza kuelezwa siku nyingi mno.Baadhi yetu tulioko nyumbani tunafahamu.
Yapo mengine ya wizi wa dhahabu.
Lipo la kusikitisha la madini ya Tanzanite.
HOMGERA BBC. MMEMSAIDIA KUMKUNBUSHA RAIS WETU.
-
Comment #8
(Posted by Mohamed Ali)
Unrated
Siku zote Tanzania inataka isifiwe na isikosolewe, ukweli ni chungu kama shubiri lakini tukikosolewa tukubali
-
Comment #9
(Posted by Richard)
Rating
    
any how hao ndio ndugu zetu walioko nje, bahati mbaya sijskiona kipindi hicho so I have no comments, may be if we get the recorded one that will be better
-
Comment #10
(Posted by Ruhangisa)
Rating
    
Jamani mlioko Uingereza jitahidi leo au kesho au siku yoyote karibuni kurecord hicho kipindi na mtutumie huku nyumbani kusudi mambo yawe wazi hata kwa viongozi wetu, waelewe linaloendelea na wachukue hatua mathubuti kurekebisha hali hii ambayo sasa si siri tena bali ni suala wazi kwa kila mtu duniani. Kuzoea kusifiwa tu ndo kunawafanya wengine walalamikie hiki kipindi na kukiona kibaya lakini sehemu nyingi duniani zimeendelea kutokana na kuchukua hatua mathubuti dhidi ya maovu Fulani ambayo yanafichuliwa na watu au taasisi mbalimbali zinazojitegemea, ili mradi si umbea ni ukweli.
-
Comment #11
(Posted by Said Kiroboto)
Rating
    
Kama kuna movu ambayo yako kinyume na maadili yetu, hilo sio jambo zuri ni kutuzalilisha, lakini je yalioonyeshwa ni ya kubuni au ni ukweli uliopo, kama ni ukweli basi sio jambo baya katika jamii kufumbia macho unyanyasaji basi hilo ni jambo baya zaidi kuliko hilo tunaloliona kuwa ni baya kuonyenshwa kwa maovu yetu, ajira kwa watoto wadogo ni kitu kinachopigwa vita sasa duniani kote, juzi niliona program moja kuhusu ajira ya watoto nchini india kwa kweli inasikitisha nakan utaiona unaweza kusema nitatoa kila kicho changu kuwasaidia wale watoto jambo ambalo hutaliweza kwani idadi ya watoto ni kubwa kuliko hata uwezo wako ulionao, katika program hiyi hiyo wakaonyesha nchi moja ya west Afrika togo watoto wanafanyishwa kazi masaa kumi na mbili kwa ujira usiojulikana tena kazi ngumu kuchekecha udongo katika maeneo ya machimboni wanaporudi nyumbani wamechoka wala hawana muda wa kukoka wanachokifanya wanjikosha vumbi wanalala kwa matayarisho ya kesho watoto hao wanahitaji elimu kama watoto wengine wanahitajika kuwa taifa la kesho kwanini watoto kama hao wawe muhanga katika maisha yao wakati kuna watanzania wanagapi hawana ajira na wana uwezo wa kufanya kazi hizo wawatumie watoto wadodo maana ya wadogo.
hili sio jambo la kusikitisha kukaa katika nchi za ulaya nakutaka kuona kusifiwa kwa nchi zetu wakati kuna madhila mbali mbali, kama ni kuzuri na kusifa za kutosha kwanini tunakukimbia nasi tusikae kule tanzania kama wenzetu
-
Comment #12
(Posted by Yahya Ali Madenge)
Rating
    
Kwa tuliobahatika kuishi kwa muda mrefu kwenye nchi kama India ambapo kuna uozo mwingi wa kijamii, jinsia na ubaguzi hatusituki sana kwa ukweli. Tena bahati nzuri zaidi kule vipindi kama hivyo pamoja na kurushwa nje ya nchi yao, pia hurushwa moja kwa moja nchini kwao na wenyewe wakaviona. Wenyewe kwa raha zao husema tu "No problem, this is India, everything is possible".
Kwa upande wetu, kama yana ukweli basi tuyaone kuwa ni kero na tuyatafutie ufumbuzi. Kama ni uongo, naungana na kila mmoja anayelaani uongo huo.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
-
Comment #13
(Posted by Nemes Makembe)
Rating
    
Mwandishi wa makala haya amenichanganya sijaelewa tatizo liko wapi. Waandishi wa habari wana fursa ya kueleza wanaloliona kwa lengo la kueleimisha jamii.
-
Comment #14
(Posted by said)
Rating
    
Mimi sioni ubaya wa kuonyesha hali halisi na ndivyo ilivyo. nimewahi kuishi kanda ya ziwa na kuona hali hiyo.tatizo la watanzania na maofisa wa afya suala la usafi hawalizingatii.kuna sheria kadha za kuzuia uchafu lakini wahusika hawzisimamii.ni matumaini yangu kuwa awamu ya nne itabadilisha hali hii ili mradi sisi wananchi tumsaidie rais wetu.
-
Comment #15
(Posted by an unknown user)
Rating
    
kama hayo yanayoonyeshwa ni kweli na siyo ya kufoji, hakuna haja ya kulalamika. Tujirekebishe na kuweka mambo sawa. Kwanini tujisifie uongo?
Mwandishi anasema kuwa habari imelenga kuchafua jina zuri la Tz kwa makusudi. Kama wewe ni mchafu na mtu akakwambia kuwa uu mchafu, kakuchafua au kakusaidia? Hii pia ni changamoto kwa vyombo vyetu vya habari vya ndani. vilitakiwa viwe vimepigia kelele jambo hili siku nyingi ili kuisaidia serikali kuamka na kuyafanyia kazi. tunajua jinsi ambavyo Serikali inavyo taharuki habari mbaya zinapoandikwa magazetini au kutangazwa katika vipindi vya TV. Mwanza ni sehemu muhimu sana ya uchumi wetu hivyo tusipuuzie jambo hili.
Na hiyo ni sehemu ndogo tu ya maeneo ambayo kwa kweli Serikali ya awamu ya nne inatakiwa kuarekebisha haraka ili kurudisha heshima ya nchi na kujenga uchumi imara. Na wananchi pia tusaidie maana ni nchi yetu na maendeleo ni yetu. Tusikubali kuwahifadhi viongozi wasanii. Mh Dialo, Mh. Ngasongwa na Waziri wa viwanda na biashara, Mh Mramba; wawajibisheni wazembe na wahujumu. msimsubiri Mh Waziri Mkuu kufanya kila kitu. Tanzania ni yetu TUIJENGE hata kama siyo kwa ajili yetu basi hata kwa ajili ya watoto na wajukuu zetu.
-
Comment #16
(Posted by an unknown user)
Rating
    
Wacheni ushambenga! Tutumieni hiyo kanda iwe kielelezo ili ukweli/uongo uwe bayana.
-
Comment #17
(Posted by Erasto Mbugi)
Rating
    
Mimi nadhani kama kuna ukweli ndani yake, lazima mambo yawekwe wazi. Kwa nini tufurahie mazuri tu na yale yasiyofaa tuyaweke kapuni? Nafikiri dosari kama hizo zikiondolewa tutakuwa na haki ya kujivunia sifa nzuri zinzazoitangaza Tanzania. La sivyo ni kujidanganya tu!
-
Comment #18
(Posted by Neila)
Rating
    
I think people have to realize that in any country, there is a good part and a bad part...showing worse things about a particular country doesnt help but destroy.
..what is the implication of my action?? is an important question to ask yourself before doing anything
-
Comment #19
(Posted by danieli Msuya)
Rating
    
I dont think there is a country where everything done is perfect as living in heaven. Every one has got his own defect but yes they can be reversed. So that is what is required. If it has happened its all over make it a history.Write a new story
-
Comment #20
(Posted by Tanzanian)
Rating
    
Ukweli ni kichomi, huuma sanaaaa!!! Lakini everyword said is nothing but the truth.Ikuwa swala la Samaki, Silaha, Rushwa, Prositution (Wanawake wanavyojiuza mjini (center of City) Mwanza au aliyo ongeza kaka Benard kuhusu kinyesi kutuka milima ya Bugando.
Na sisituna omba kuona kipindi hicho.
-
Comment #21
(Posted by Assaa)
Rating
    
kama hayo yametokea basi na sisi tuwe tayari kuyatangaza yao mabaya. Kwa vile yanajulikana nyinyi ndio muayaanike hadharani ili na wao wajue kuwa ni wachafu.
-
Comment #22
(Posted by Arnold Njau)
Rating
    
Kimsingi inabidi tuwashukuru BBC tena na kuwapongeza kwa programu hiyo inaonyesha vile ambavyo vyombo vya habari hapa nchini vimelala kabisa vimebaki tu kuandika mambo ya siasa na na mambo ya kusifia ouvu kuacha kuandika mambo yanayo gusa jamii, kama hayo kweli basi ni wakati wa kuliangalia hilo na si kulalamika lalamika na si minofu tu ya samaki hata mazingira ya nyama za ngombe kuku kwakweli hayafai kabisa si wakati wa kusifiana tu bali uwajibikaji kihalisi unatakiwa. Aksante BBC rusha hewani tena wengi tukione wanacho lalamika wabongo wezangu..
-
Comment #23
(Posted by ndessario)
Rating
    
sasa mnabisha nini?mbona hayo ni kidoo tu?tena inaelekea huyo mwandishi ni mzungu ndio maana hajkuonyesha jinsi madini yanavyoibwa!
haya ni mambo ya kweli kabisa
kinachotakiwa kufanywa ni kukubali ukweli na sio kulaumu,
watanzania tuamke sasa mambo ya kubebwa sasa mwisho!!!!tukubali ukweli, kila mtu au kitu chochote kina uzuri na ubaya wake bwana,.
-
Comment #24
(Posted by Adventina)
Rating
    
Mimi ninaunga mkono walionyesha ukweli uliopo Mkoani Mwanza. Kama samaki sato wanaotoka Mwanza kuja Mikoa mingine wanawekwa dawa ya kuzuia maiti izioze ili hao samaki wasioze badala ya kusafirishwa kwenye magari yaliyoruhusiwa kubeba samaki wabichi kwa ajili ya kujinufaisha wenyewe kibiashara wakati wanaangamiza wananchi wa Tanzania. Maradhi ya ajabu yanaendelea kuwapata wananchi hapa nchini na hakuna anayefuatilia kwa kula samaki hao ambao wanasafirishwa kwa wingi kama mabero ya nguo za mitumba. Tunaomba serikali ilishughulikie suala hili kabla ya kukanusha ukweli uliopo kwenye habari hii.
-
Comment #25
(Posted by cheche)
Rating
    
bahati nzuri au mbaya nimeona nusu ya mwisho ya kipindi hiki, na sidhani kama kuna udhalilishaji wowote bali ni hali halisi ambayo serekali inatakiwa iitupie jicho
-
Comment #26
(Posted by Dr. Erick Urio)
Rating
    
Huku ni kudhalilisha . Mimi nafikiri wangekuwa wazuri wangewasiliana na hao wanaoitangaza Tanzania hapo london. Wanatakiwa waache UNAFIKI na kuongea UKWELI wa mambo maana wale watoto hawakuhajiriwa na mtu ye yoteila wanajitafutia risiki zao tu. Hapa naamini UJUMBE UMELETWA vibaya na wahisika!
-
Comment #27
(Posted by Makomba Frank)
Rating
    
Watanzania sasa tuamke, tuache tabia ya kupenda kusifiwa tu , vilevile tujifunze kukosolewa.
Mimi binafsi na kama maoni ya walio wengi , sioni ubaya wa kuonyeshwa kipindi hicho. Hiyo anaonyesha ni jinsi gani vyombo vya habari hapo nyumbani na viongozi hawaoni umhimu wa mambo kama hayo tuliyokosolewa na BBC.
Utunzaji wa mazingira na usafi wake ni mhim pia kwa kwa jamii, lakini kwa vile viongozi wetu wanao ajibika hawajali. They are corrupt minded.
Kuna mengi sana ambayo inabidi tukubali mfano rushwa, wizi wa mali ya uma; au tuseme kuteketezwa kwa eka 10000 za miti ya Mihama huko Mwime wilayani ya Kahama siyo ubadhilifu wa mazingara? Tukiambiwa ukweli tunachukia!!
-
Comment #28
(Posted by Justine)
Rating
    
Watanzania tuache kulalamika; walichoonyesha BBC ni ukweli halisi wa mambo. BBC wameonyesha upande wa pili wa shilingi ambao viongozi wetu hawataki ujulikane.
Kama tunataka maendeleo ya kweli, tuache unafiki. Huu ni muda wa kuita Sepetu kuwa sepetu na si kijiko kikubwa!
Na hao wanaodai kipindi hicho kikomeshwe, kitakomeshwa kivipi. Hapa Uingereza tuko dunia nyingine kabisa na sio kule bongo ambapo leo serikali ikijisikia inapiga marufuku kipindi au gazeti fulani kama ilivyotokea kwa HAKIELIMU kwa kutoa upande wa pili wa elimu ya msingi bongo!
Wabongo amkeni na kujiuliza ukweli ni upi na si kulalama!
Kipndi nimekiangalia, mbaya zaidi nikiwa na Flat mates wangu na kilinisikitisha. Yamkini Walichoonyesha BBC si zaidi bali ni kweli, ukweli mtupu wa wanayojiri bongo. Nenda Mwanza utayaona yote mchana kweupe!
-
Comment #29
(Posted by Alphaxard Lugola)
Rating
    
NIMESOMA UJUMBE HUU KWA MASIKITIKO MAKUBWA SANA. NAKUBALIANA MOJA KWA
MOJA NA MAONI YA DAKTARI ALIVYOTOA. AIDHA NAJIULIZA, SHERIA YA UPIGAJI
PICHA TANZANIA IKO WAPI? LIKIZO? NINA UHAKIKA HIZO PICHA ZIMEPIGWA NA
WAGENI. LAKINI PIA KUNA MTANDAO WA WATANZANIA AMBAO WANALIPWA PESA
NYINGI NA WATU WA NJE ILI WAWAPIGIE NA KUWAPELEKEA HIZO PICHA KWA AJILI
YA SHUGHULI KAMA WALIYOIFANYA.
-
Comment #30
(Posted by Mnyika)
Rating
    
Was it a documentary or commentary on "Darwin Nightmare"?
-
Comment #31
(Posted by Gerson Fumbuka)
Rating
    
MIMI SIELEWI TATIZO LIKO WAPI. KUNA MATATIZO MAKUBWA SANA KULIKO YALE
AMBAYO YAKO KWENYE HIZO SIJUI PICHA.
NCHI HII INA MASHGA KIBAO HAYA NDIYO MATATIZO YA KUYAZUMGUMZA. HAYA
NDIYO YATAASILI KIZAZI KIJACHO NA SIYO PICHA PICHA PICHA. TUNATAKIWA
TUFUNGUKE KIMAWAZO. KINA MSEMO UNASEMO MFICHA UCHHAZAI. TUONGEE HOJA
NZITO ZA MIAKA IJAYO BWANA
UPANDE WA HELA
-
Comment #32
(Posted by capt. khalil M. I)
Rating
    
SAWA LAKINI UKWELI UNAUMA SANA!!
HAKUNA SIRI AU UONGO KATIKA HABARI ILIYOTOLEWA LONDON.
KUNA JAMBO GANI KIPYA AU ITAKAYOWEZESHA WANANCHI WA TZ KUENDELEA NA KUISHI MAISHA
MAZURI, SERIKALI YA TZ IMETUANGUSHA NA UONGO MWINGI TU.SIONI HUKO TUNAKOENDA!!
MAKABURU NDIO HAO WAMEINGIA KWA FUJO NA KARIBUNI NCHI ITAKUWA IMETAWALIWA NA WAZUNGU
WACHACHE NA SIO RAIA WA TZ WATAKAO MILIKI ARDHI -MADINI, MASHAMBA, MAHOTELI NA
VIWANDA NCHINI....USIOGOPE WACHA WATUSEME, UKWELI NDIO HUO...
-
Comment #33
(Posted by Onesmo Kyauke)
Rating
    
Nisingependa litumiwe neno "Kudhalilisha"
Nadhani kubwa tujiulize kama yaliyosemwa ni ya kweli au la. Kama ya kweli
tujirekebishe, kama ya uongo basi tulalamike.
-
Comment #34
(Posted by t_tonga)
Rating
    
ukweli unauma hakuna cha uongo kwani hata mimi nimekiona unataka yatangazwe mazuri tu sasa kama mabaya hayatangazwa watu watajuaje mabaya ni boraya yaonekane ili watu wajue tabia ya kufichana sio nzuri walio yaonyesha ni yakweli na sio ya kuzua watoto wanagombea wali kwa maharagwe wengine wanalala nje jamani hamuachi nyinyi kweli samaki wanatoka mafunza hata yule bibi amepoteza jicho kwa harufu ya gas ya samaki
-
Comment #35
(Posted by nkurufi)
Rating
    
Sio uungwana kwa hao bbc kujipendekeza na matatizo ya nchi yetu kwani inawapa faida gani?Tunajua kuna matatizo kwetu na ni mengi tunachotakiwa kufanya ili kurekebisha ni kubadilisha viongozi wazembe na tunatatua shida zetu wenyewe kwa awamu na hii sasa ni kasi mpya itayaweza yote ila lakini ni kwa nini bbc wasiyatangaze ya kwao huko ulaya kuna maovu mengi tu huko kama gereza la au jehanamu la Gwanatanamo bay.Misukosuko ya south Ireland na utumiaji wao wa madawa ya kulevya nguvu za nyuklia kwa nini wasiyaseme hayo ya kwao?hatutaki kimbelembele bbc chunguzeni ya uozo wa uingereza na marekani kwanza huko ndio wanaongoza kusafirisha silaha kuleta africa ili kufadhili uovu na kuiba mali za africa na kuhatarisha amani somalia,D.R Congo,Sudan,Irak nk,pia biashara za ukahaba hata kwa watoto na u uzwaji wa binadamu yote hayo bbc yapo huko ulaya kwenu mbona hamuyatangazi mnakuwa tu vibaraka wa ukoloni mamboleo?sasa watanzania wenzangu kuna methali ya kiswahili isemayo nyani halioni kundule
-
Comment #36
(Posted by JANUARY)
Rating
    
Mimi ndhani yaliyo andikwa humu ni changamoto, kama sliha zinaweza kuingia kienyeji tu bila watu wa usalama kujua hii ni hatari, pia hata hayo mengine yaliyo zungumzwa mengi yapo hapa kwetu. pia ningeshauri hii heading iliyotumiwa siyo kweli tumezalilishwa haya mambo yapo na syo mwaza tu, watu wa nje wakitunanga hivi nafikiri tuta chukua hatua muafaka.
-
Comment #37
(Posted by Msanii)
Rating
    
Ni kweli inauma na kama tujuavyo kuwa ukweli unauma. Ila nadhani ni changamoto kwa serikali yetu kuwa makini zaidi katika usimamiaji wa haki na maisha bora kwa watanzania. labda tujiulize, ni kweli hakuna sexual workers Tanzania? Ajira kwa watoto je? Pia naamini kuwa mtayarishaji wa kipindi hiko amejaribu kuionesha dunia madhara ya kuingia mikataba ya kimataifa kichwa klchwa. kwa upande mwingine ni hatari kwa usalama kwani kama kiwanja cha ndege Mwanza kimegeuzwa kuwa transit ya silaha basi nadhani tujisafishe kwa hilo. TUSIWE WASULUHISHI KWA MIGOGORO AMBAYO SILAHA ZAKE ZINAPITIA KWETU. Serikali ikanushe au kuthibitisha ili tujue ukweli.....
TUJISAHIHISHE.
-
Comment #38
(Posted by jahawaswol)
Rating
    
hakuna tatizo kusema ukweli pale panapostahiki lakini mwandishi ana hakikutangaza yale yote anayoyaona lakini wengi wanajaribu kutoa taarifa kinyume kabisa
-
Comment #39
(Posted by Badru Adam Ali)
Rating
    
Ukweli utabaki ukweli na uongo uchukuliwe hatua kwa yale waloyaandika.kama kweli basi tunaomba serikali kuyafanyia kazi na kuyarekebisha ili Tanzania iweze kusifika kwa kuwa nchi nzuri yenye amani na mazingira mazuri kwa wawekezaji.lakini kwanini wameonesha mabaya matupu na hawakuonesha mazuri na halafu kuyapima yapi ni mingi zaidi.Yaonesha mwandishi amekusudia zaidi kubomoa kuliko kujenga.
-
Comment #40
(Posted by F.Chagula)
Rating
    
BBC nawasifu kwa kuonyesha ukweli wa mambo yalivyo huko Tanzania. Mimi sishangai kwani ni kweli tupu wala si uwongo. Wabunge hayo hawayaoni ila wanadai waongezwe mishahara. sawa acha watu wa nchi za nje waonyeshe jinsi watanzania tulivyo, uwongo, umalaya, chuki, rushwa, n.k. namuo,mba Rais wa sasa afatilie na kuleta mwamko wa hali halisi ya nchi na ikiwezekana Tanzania ianze kuona makosa inayofanya na kujaribu kurudisha demokrasia ya kweli.
Mimi sishangai BBC, mwaka 2001 nilikuwa Geita nikaona kila siku zaja ndege kuchukua vidonge vya dhahabu, lakini zinakokwenda na anayepata faida Mungu ndiye anajua. Je hayo ndo maendeleo ya Mwafrika angalia nigeria watu mpaka wamefikia hatua ya kukata mabomba ya mafuta angalau nao waambulie kidogo hiyo maliasili ya taifa. BBC endelea kutoa habari za namna hii. Tarehe 22 nakuja huko Tanzania na tarehe 26.6 nitaelekea mwanza kwa ndege then na mimi nitajionea hayo yaliyorekodiwa na BBC.
-
Comment #41
(Posted by Chacha)
Rating
    
Hivi ni lini Watanzania tutaacha UNAFIKI?Tumeishi kinafiki sana siku zote.Watu wanaonewa,madini yanavushwa kinyemela,silaha zinavushwa,madawa ya kulevya hapa Tanzania ndio Centre yaani uovu wote unaofanyika huko ughaibuni hapa pia unafanyika.Kwa hiyo wacha tu BBC wakionyeshe hicho kipindi ili kama kitaandhiri uchumi wacha tu kiadhiri ili serikail ichukue hatua za haraka.
-
Comment #42
(Posted by Edward M.Moshi)
Rating
    
Hullo Dear Tanzanian,
Hili jambo la nchi yetu kutangazwa vibaya huku Uingereza si jambo zuri. Lakini inabidi tuwe waangalifu sana katika kuamua maelezo yetu. Kwanza lazima tuone kama jambo lilliloandikwa ni sahihi au la. Pili Kama kuna ukweli ni lazima viongozi wanaohusika katika kuliweka soko la samaki Mwanza kuwa safi wawajibishwe bila kuwaonea huruma.
Kwa mamoni yangu ningeomba ninyi wenzetu mliko nje mtusaidie pia kutoa maoni yenu kwa viongozi wetu na muwe wakweli kuwaeleza ili wahusika wote wachukuliwe hatua kali za kinidhamu.Naomba mjaribu kufanya hivyo kwani Raisi wetu Mh.Jakaya Mrisho Kikwete hana mchezo na viongozi wazembe na wababaishaji. Ahsante kkwa kutujulisha sisi ndugu zenu yanayoendelea huko London. Napenda kukuarifu kuwa mimi ni mfanya biashara ya mambo ya Utalii na kwa wakati huu niko mjini Moshi na sijabahatika kufika Mwanza sasa ni zaidi ya miaka mitatu tangu nitoke huko. Karibu sana Upande Mlima Kilimanjaro na Safari za mbuga za Wanyama pia Ufukwe mzuri wa Zanzibar na Mafia.
Ahsante,
Edward M.Moshi
-
Comment #43
(Posted by Lameck Noah)
Rating
    
Naona kuwa wanataka kutumaliza hivyo kuanzia sasa tugome kusikiliza BBC redio na kuangalia TV yao.
-
Comment #44
(Posted by mahamudu y.mohamed)
Rating
    
binadamu hubadirika kuambatana na mazingira aliyomo.kila mazingira yana ualisia wa maisha ya binadamu kwa wakati huo.Wengi wa sisi watanzania tuliokulia vijijini na mpaka sasa tulikwenda na tunakwenda shuleni bila viatu.Lakini mtoto aliyezaliwa mjini dare salaam, maeneo ya masaki.ajawai kufika kijiji chochote nchini.siku akifika akaona wanafunzi wanaenda shule bila viatu.atashangaaa sana.Vile vile wa kijijini akija mjini atashangaa.Huo ndio uasilia wa mazingira na binadamu.Yaliyomo kwenye hiyo artile ni ya kweli na yapo mwanza yanafanyika.Kwa ulaya itakuwa ajabu maana hata watoto wenu hawayajui hayo mazingira.Je mlitaka waonyeshe barabara nzuri.ikulu na majumba mazuri ya ppf tower.Ualisia wa jambo ndio msingi wa kupata mwekezaji mzuri mwenye haja ya kuwekeza na kuwasaidia watanzania .Tumeona wawekezaji wanaokuja,migogoro chungu mzima.madini mmeona.sasa hao ndio wawekezaji wanaotaka! tuwaonyeshe danganya toto.Huku hali mbya sana kwa mtu wa chini.maisha yake ni duni.wanaishi kwa mapanki.je mlitaka dunia ionyeshwe nini,migodi ya madini.naomba muwape ualisia wa mazingira tuliyomo,asilimia kubwa watanzania wanaishi kwa umasikini wa kutupwa.mkiwadanganya kesho watakuja,alafu wawaulize mbona mmetuambia watanzania wanaishi kwenye neema,leo mnasema mnaitaji mrahaba.naipongeza bbc kwa kutoa ualisia wa mtanzania na mazingira aliyomo. labda juhudi za makusudi zitachukuliwa kuwainua watanzania kiuchumi waache kula mapanki,
-
Comment #45
(Posted by Mathew)
Rating
    
Tanzania imedhalilishwa kwa lipi? Je hizo picha hazikupigwa hapa Tanzania? Kama hizo picha zimepigwa hapa kwetu na ni za kweli basi tungewapongeza hao BBC kwa kuyasema na kuyaonyesha ambayo vyombo vyetu vya habari vinajidai haviyaoni. Sidhani kama kuna la kusikitikia kwa kuonyeshwa kipindi hicho. Naamini huu ndio wakati wa kuachana na utamaduni wa kuangalia upande mmoja tu wa shilingi. Kama BBC wameonyesha ule UKWELI wa upande wa pili
basi ni vyema na haki. Hilo lilipaswa kufanywa na Television ya Taifa ikiwa kama kioo cha jamii ili tujione tulikopungukiwa na tukajisafisha.
Kuhusu swala la silaha. Je mwandishi wa makala hii hajui kuwa Tanzania ya leo si ile ya 1980? ambako wizi wa kutumia silaha kama ilivyo leo ulikuwa kidogo sana? Je, silaha zinatoka wapi ambazo zimekuwa zikitumika katika ujambazi wa mchana kama ule wa Ubungo? Imewezekanaje LMG ikatumika Ubungo na isipatikane? Hayo yote kama yamewezekana, je la biashara ya silaha haliwezekani?
Nawapongeza sana BBC kwa kuanika ukweli wote ili ikiwezekana tubadilike.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
-
Comment #46
(Posted by henoko abraham)
Rating
    
Ninaimani kuwa baadhi ya wachangiaji wa maada hii hayamkini hata hiyo film au kanda hawajaiona.mimi naishi marekani na nimeiona hakuna jambo lolote ambalo halina ukweli ndani yake.Vijana wa kike wanaofanya uasherati kwa ajili hapo?yule dada aliyepigwa kisu siyo kweli pale mwanza ?yule mwalimu wa shule aliyesitahafu hakueleza kweli?na mengine mengi tu,wale marubani wakirusi maneno waliyokuwaakiyasema si yakweli nani anapinga hayo?.kwa taarifa yenu filamu hiyo siyo documentary ya BBC,ni ya kikundi cha watafiti walioko University moja hapa Amerika ambao wameamua kuwasaidia kufunua mambo machafu yanayoendelea ambayo watanzania wengi hawajajui.Msemaji mmoja amesema kuwa filmu hii imechukuliwa kwa siri je mkuu wa mkoa naye alichukuliwa kwa siri.
USHAURI:
Kabla hujasema kitu kuhusu hii kanda pata nafasi ya kuiona na ndipo utoe maoni yako watanzania tufike mahali tuwe wakweli acheni propanganda za siasa(SI HA SA) na hali halisi ya maisha hilo ndo linatuponza na litaendelea kutuponza.
-
Comment #47
(Posted by paschal mulimila)
Rating
    
Tunashukuru sana kwa watanzania wenzetu mlio huko na kuona kipindi hicho kilichorushwa na BBC. Hata mimi niliposoma hii habari imenistua sana kwani siwezi kuamini kaka watu wa BBC wanaweza kurusha matangazo mabovu kama hayo ninachoomba Serikali ifuatilie kwa makini na kama kweli hii imefanyika bila ridhaa ya serikali hatua kali zichukuliwe kwani inataka kutuharibia amani yetu tuliyoweza kumudu nayo kwa muda mrefu. Tunawashukuru sana ndugu zetu mnaoishi huko kwa kutoa ushirikiano.
-
Comment #48
(Posted by Agnes)
Rating
    
Acha waseme ukweli itasaidia labda tutajirekebisha
-
Comment #49
(Posted by James D.Rugangila)
Rating
    
Habari,Kwa kweli habari hii ni ya kusikitisha sana,kwa mawazo yangu ni kwamba kazi hii ya kuchafua nchi ya Tanzania itakuwa imefanywa na sisi watanzania kwa kushirikia na BBC ambayo makazi yake ni Londan,watanzania sasa tunaelekea pabaya,kwani hata kama hayo mambo yapo haikuwa sahihi kuyatoa nje badala yake ingekuwa ni bora kufanya kazi ya kuishauri serikali,kwani hakuna mtu hasiyependa maendeleo katika nchi yake,zaidi ya hapo ningependa kuimba serikali kuchukua hatua kali za kisheria kwani tuna uwezo wa kulishtaki shirika la utangazaji la BBC kwa kujaribu kuichafua nchi.
-
Comment #50
(Posted by Maria)
Rating
    
Watu weupe wabaya sana wanajitafutia umaarufu katika mambo madogo ambayo kila mahali yapo hata ulaya na kujifanya wakweli mbona wizi wao wa mali za nchi za afrika hawaweki wazi? Hebu waondoe maboriti yao kwanza kabla ya kukiona kibanzi chetu
-
Comment #51
(Posted by mbongo)
Rating
    
Mimi nimekiona hicho kipindi. Ninakubaliana na wale wanaosema kua kipindi hakijaidhalilisha Tanzania bali kimeonyesha ukweli. Umasikini ndio chanzo cha nchi yetu kukubali sangara (nile perch) kuwekwa katika ziwa la Victoria. What we have seen are the effects of that action. The fish has become an ecological disaster and other effects are unemployment which leads to pristitution and the rest of it...
Katika hicho kipindi kuna pilot mmoja mrusi alisema... mambo yote haya ni sababu WATANZANIA WAVIVU. Mbona hii kitu haijaongelewa, ati kama tusengalikua wavivu tungejaribu kuondokana na effects za sangara...what do you think?
-
Comment #52
(Posted by an unknown user)
Rating
    
waswahili wanasema mficha ugonjwa kifo kitamuumbua. kama hawataki hali halisi kwa maskini tanzania ijulikane wafanye kitu kurekebisha hali hii basi. maendeleo ya teknologia na majengo makubwa ni mjini tu na hata hapo mjini watu wanateseka sana. utalii na haya makampuni yanayokuja nchini hayasaidii kila mtu. tutakapolikubali tatizo tu ndio tutakapoweza kupigana nalo hivyo kwanza serikali yetu ikubali tatizo hili na ndipo hapo tu watakapoweza kupigana nalo.
-
Comment #53
(Posted by alex)
Rating
    
sidhani kama wakileta hiyo film itaonyeshwa hapo tanzania,it was a good programme na imesikitisha sana lakini ndio hali halisi hapo mwanza i guess watu wachache wanafaidika na business ya sangara na wengineo wengi wanakufa njaa.what a shame.!
-
Comment #54
(Posted by an unknown user)
Rating
    
wale samaki wangewez akusaidia jamii ile ila utakuta kuna mkubwa kapata ten percent hapo hivyo ndo wale watu wanapewa monopoly kuexport samaki na wananchi wanabakia kula mifupa ya samaki na mkia. sharti serikali yetu ijaribu kutupenda, kutuendeleza na kutusaidia wananchi wao na hivyo kutufikiria kwenye policy zao na kutowapa makampuni monopoly kwenye maeneo fulani iwe madini, utalii au sector nyingine yeyote
-
Comment #55
(Posted by Dileku Kumpasi)
Rating
    
Kama hivyo ndivyo inabidi kuwa makini na waandishi wa habaritoka nje na hata wazawa ambao hawaitakii mema nchi yetu.Pia watalii, biashara huria isiwe ndio sababu ya kuwaachia watalii kuvinjari na kufanya lolote walitakalo ndani ya nchi yetu. Na kwa wananchi pia tuwe makini na wageni na yale wayafanyayo.Tusikubali kudhalilisha cnhi yetu kwa hali yoyote ile.
-
Comment #56
(Posted by msisi)
Rating
    
Mimi nadhani tukubali kuwa mshahara wa dhambi ni mauti na faida ya uchafu ni kuchekwa hivyo tukubali yote.Kwani hakuna anaejua kuwa sangara huenda nje na watanzania kula makapi ya sangara ambao walionyeshwa wakianikwa.Kama ni hao funza kweli kwani uongo nani asiejua malalamiko ambayo watu wengi walikuwa wakisema dawa ya kuhifadhia maiti inatumika kuhifadhia samaki na hili likioneshwa tutasemawametuonea?
-
Comment #57
(Posted by GODFIELD)
Rating
    
Neno kudhalilisha litakuwa na maana iwapo unayeambiwa hauko hivyo.Katika hali halisi hivyo ndivyo ukweli ulivyo,inachopaswa wahusike waelewe kwamba yahitajika mabadiliko.Watanzania tukubali ukweli bila kujali unatufurahisha au la.Mfano suala la ubinafsishaji ambavyo lina kasoro,watanzania tunanyanyaswa sana, lakini viongozi wetu wanahubiri mema tu, bila kusema mabaya yaliyopo.Tutaendelea kudanganyana hadi lini? Mfano Viwanda vya sukari nchini vinavyoendeshwa, inasikitisha wahusika wanahubiri tofauti, akisema mtu/chombo ukweli ulivyo anaandamwa, anaita TUNADHALILISHWA.Cha msingi ni KUBADILIKA. Rais wa Awamu ya nne tunakuomba na serikali yako tupieni macho uendeshaji wa viwanda vya sukari hasa cha MTIBWA.
-
Comment #58
(Posted by mambopoa)
Rating
    
heko bbc hamkuidhalilisha Tanzania mmeufichua ukweli ingawa shubiri ni chungu na tuinywe tu mpaka viongozi mtakapoirekebisha tanzania,Tanzania yetu ni nzuri lakini tumeitupa inafika hata watoto kufanya kazi hii inasikitisha sana labda sasa viongozi wetu wataibuka katika usingizi mzito waliolala maana ni aibu hii sasa na maji yakimwaika hayazoleki heko bbc mzidi kufichua mabaya zaidi mengine ambayo sisi wananchi wengine hatuyajui hongera bbc.
-
Comment #59
(Posted by Ferdinand Mgaya)
Rating
    
Naamini kilichoonyeshwa kinaweza kuwa na ukweli kwa kiasi kikubwa. Hao ndugu walioko ulaya siamini kama wanaijua Mwanza na mambo yanayotokea hata wakadiliki kusema filmu hiyo haina ukweli, kama wanaijua Mwanza basi wanaijua mwanza ya watu wa kima cha juu (Capripoint,buzuruka n.k)nendeni makoroboi na maeneo yanayofanana na hayo. hivyo vichwa haviishii Mjini Mwanza vinauzwa vijijini pia.Naomba tukumbuke kisa cha mfalme aliyesifiwa kuwa amependeza na watu wazima katika himaya yake mpaka mtoto mdogo alipomwambia ukweli kwamba mfalme uko uchi na ndipo mfalme alipoenda kuvaa nguo na kuijisetili.Naomba hao ndugu zetu walioko majuu wawe wakweli kusema juu ya hali halisi ya Tanzania kwani tunaweza kuwanyima haki ya kupata misaada ndugu zetu kwa sababu ya unafiki na kujifagilia kusiko kuwa na maana. tukumbe Mficha maladhi kifo humuumbua.
-
Comment #60
(Posted by Burton Twisa)
Rating
    
Filamu hiyo nimeiona miaka miwili iliyopita lakini nilikuwa nasikia kwa watu wengi wakiizungumzia kabla sijaiona. Kwa hiyo siyo ngeni sana na ilichukuliwa wakati wa awamu ya pili au ya tatu. Tukubali kuwa suala la minofu ziwa victoria halieleweki, na ikumbukwe kuwa kuna waziri alilazimika kujiuzulu kwa sababu ya hiyo hiyo minofu na sijui kama serikali ilichukua hatua zaidi ya hapo kuwashughulikia wahusika kabisa katika hujuma hizo. Serikali ya awamu ya nne pamoja na kushughulikia usimamishaji wa filamu hiyo lakini lazima iangalie kwa undani mambo yanayofanyika ziwa victoria na viwanda vya minofu pamoja na uthibiti wa uwanja wa ndege wa Mwanza.Nafahamu filamu ni chafu kwa jina la nchi yetu,na uchukuaji wa picha hiyo unakiuka haki za binadamu na wanayoyafanya wafanya biashara mwanza (minofu ya samaki) wanakiuka haki za binadamu. Je ni wapi tuanzie kusahihisha hilo?
-
Comment #61
(Posted by H. Kiisnzah)
Rating
    
very nice tanzanian government must react to suxh bad tv programs and the like.
-
Comment #62
(Posted by MIKE PIMA)
Rating
    
ITABIDI HIKI KIPINDI KIKOMESHWE MARA MOJA
-
Comment #63
(Posted by Nyinisaeli)
Rating
    
Mie nadhani hii si nzuri lakini pia katika utandawazi huu tulio nao nadhani issue ni kujirekebisha pale ambapo tuna mapungufu kuliko kupambana. Kwani ukeli hubaki kuwa ukweli. Kiukweli kiwanja cha Mwanza hakina control kwa abiria hasa wanaoingia manake kama wanaotoka kibondo, kasulu, kigoma na ngara ambako hakuna security check points, wanapoingia pale mwanza wanatoka kama arrivals waliotoka dar au kilimanjaro, jambo ambalo hatuwezi kuwa na hakika kama mizigo inayotoka kigoma na kagera iko salama kwa kiasi gani. We need to be honest pale ambapo tuna matatizo tujirekebishe. Ni kweli wametudhalilisha lakini hata tv zetu za ndani na maofisa na sisi wananchi wenyewe tumeyaona hayo na tumefanya nini?
-
Comment #64
(Posted by Mohammed)
Rating
    
Nashangaa kuwa baadhi yetu tunapiga kelele eti BBC inatudhalilisha. Si jambo geni kwa Tanzania kuwadhalilisha rai wake. Sisi tulioko huku nje wengi wetu tumeondoka nchini kwetu kwa sababu za udhalilishwaji tuliofanyiwa na serikali zote mbili za Tanzania na ile ya mashetani wa Zanzibar. Mimi nataka hiyo filamu iendelee kuoneshwa na wala hakuna haja ya kuipigia kelele kwani sawa kabisa ili nchi hiyo iweze kujirekebisha. Kwa nini Sky ilipoonesha mazuri matupu haikulaumiwa. Ndiyo maana BBC imetaka kuweka mizani sawa kwa kuwaonesha walimwengu maovu pia na siyo mazuri ambayo kwa Tanzania ni asilimia 40 tu yaliyo mazuri wanayofanyiwa wananchi.
-
Comment #65
(Posted by fredy laizer)
Rating
    
Naomba watz wenzangu tukubali ukweli kwa wenye kipindi hawajabuni njia ya kufanya nikurekebisha uozo huo nasikukata.mbona sifa tunapenda than kukosolewa chonde tufanye hima tutoe kashfa hiyo pls
-
Comment #66
(Posted by falesy kibassa)
Rating
    
sina shaka na kipindi hicho kwa kuwa tanzania hatufanyi mambo kwa uwazi matokeo yake tunasifiana hata pasipo na sababu. hakuna haja ya kutaka kuzuia kipindi hicho kwani kinaonyesha jinsi vile tanzania isivyo serious na mambo ya afya za binadamu, haki za binadamu, maendeleo ya nchi, uchumi, siasa na mambo kama hayo badala yake kila mmoja amekaa katika kutafuta ni nini atakifanya ili yeye na watoto wake waende katika nyumba kuu ya nyumbani.
ni muhimu kutambua wakati tanzania ikijitahidi kujitangaza nje ya mipaka yake hasa ulaya; hata nchi nyingine zinajitangaza hivyo hivyo. hivi we unashangaa nini je hujui au hukumbuki kwamba kule marekani hadi leo hii wengi hawjui k ama mlima kilimanjaro uko tanzania wakijua wazi uko kenya? je nini kilisababisha? wenzetu wanajitangaza sie tumekaa kulalamika. kalaga bao.
kampeni za uchaguzi kenya na uganda zinatangazwa hadi super sport, m-net, discovery tv lakini za tz sana sana star tv na tvt. hii ni kuonyesha kuwa wenzetu wameadvance katika kujitangaza an tanzania bado tuna ule usemi uliopitwa na wakati "chema chajiuza..."
tuache kushangaa tufanye kazi na hizi lugha za sujui alipotafutwa hakupatikana ziishe huu ni uzushi na uchongezi kwamba huyu mtu hafanyi au hashindi kazini au hana simu na kama anyo kila mara amezima kama gaidi vile.
andikeni habari zenye uyakini badala ya kukurupuka tu na majungu yasiyo na maana yoyote
-
Comment #67
(Posted by falesy kibassa - chief)
Rating
    
kama ni kudhalilishwa basi tanzania tunajidhalilisha wenyewe kwani ikiwa tunataka mambo yetu yatangazwe vizuri kwa nini tusifanye mambo mazuri ili wakutangaza watangaze.
hiyo safi sana lakini tu nikiwa mtu nayeufahamu uchumi vizuri nasikitika kwa kuwa soko la minofu ya sangara kule uingereza na kwa mataifa washirika wa hiyo haina dili tena.
tujipange upya
-
Comment #68
(Posted by Fabian Mesanga)
Rating
    
BBC hongera sana. Hivi wanaosema Tanzania inadhalalishwa wana maana gani? BBC kusema ukweli ambao wote tuliopo hapa nchini imekuwa dhambi. Ukweli ni kwamba Tanzania ina maeneo mengi ya uozo. Kwani si kweli kwamba vile vichwa vya samaki ambavyo huitwa "punk" kule Mwanza vinatumika kama mboga kanda ya ziwa na kwingineko hapa nchini? Bila hiyo punk ni wazi watu wengi wangelala njaa. Watanzania tuwe tayari kukubali ukweli na kucukua hatua za kujirekibisha ili tupate maendeleo ya kweli. Je, BBC wakiandika kwamba kila mwaka mabilioni ya shillingi huibwa serikalini tutasema ni uongo na wakati hizo taarifa hutolewa kila mwaka na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa mahesabu ya serikali?
Naomba BBC iendelee kufichua maovu mengine mengi na uozo vilivyokithiri na ambavyo watu wengi hawafahamu au wanaogopa kusema kwa kuhofia usalama wao. Hii itachangia katika kuwafanya viongozi wetu ambayo wanajali zaidi masilahi yao binafsi na jamaa zao.
-
Comment #69
(Posted by john chacha)
Rating
    
Kipindi hicho binafsi iskukiona, lakini yote yaliyoonyeshwa au kutangazwa kwa kiasi kikubwa ni ya kweli na kwa kiasi kikubwa serikali kupitia vyombo vyake mbalimbali Mwanza inazo habari ya mambo yote yaliyoonyeshwa. mfano suala la midege mikubwa na hata ndogo kutua uwanja wa ndege mwanza na mara nyingi usiku na pia kuondoka usiku limekuwa likipigiwa kelele kuwa ndege hizo zimekuwa zikitumika kuingiza madawa ya kuevya, silaha kupitia kwenda maeneo yenye migogoro na pia madini yetu kama dhahabu, almasi, tanzanite na mengineyo yamekuwa yakiporwa na kupitishwa kwa njia hiyo hapo uwanjani.Hili siyo siri. Polisi, uhamiaji, usalama wa taifa na vyombo vingine vya serikali hapo uwanja wa ndege na hata mkoani inaonesha wanafaidika ndiyo maana hawachukui hatua kudhibiti. umefika wakati watumishi wa serikali katika uwanja huo dhibitiwa ama kuhamishwa kwani wanatupotezea mabilioni ya fedha kwa ulafi wao. Ndege hizo za minofu zituwe nakuondoka mchana tu na zikaguliwe kwa kina.Kwa vile yote yaliyoonyeshwa ni ya kweli tupu sina haja ya kuyazungumzia ila tusilaumu kitendo cha bbc kuyaonyesha na kuyaweka hadharani bali yote hayo tuchukue hatua za kuyarekebisha. Hili ni changamoto kwa serikali ya mwanza na vyombo vyote vya serikali mkoani humo na hususani uwanja wa ndege.
-
Comment #70
(Posted by Nthelezi Nesaa)
Rating
    
Katika kusoma habari ya BBC nimeshangaa kwa jinsi ilivyochukuliwa vibaya au tuseme kwa upenzi. Kwani yaliyoonyeshwa ndiyo hali halisi jijini mwanza na si mwanza tu. wangeweza hata kuonyesha uoza unaondelea kwenye machimbo ya madini, maofisini hata majumbani sijui mwandishi angetumia neno gani kushangaa? kimsingi hapa tatizo siyo kudhalilisha. tunadhani kama mwandishi aliyetuma habari hii ni mwandishi, ana haja ya kujikumbusha kanuni mojawapo ya uandishi habari kuwa unalipoti mutatis-mutandis,yaani kama ilivyo.
kuna kudhalilisha gani kwa mfano kuonyesha vichwa vya sangara vyenye kujaa funza? kuna udhalilishaji gani kuonyesha vyangudoa wakijiuza jijini mwanza? kwani hawapo kweli wanaouza miili yao kwenye miji yetu? je siyo sisi wakiwemo hata viongozi wanaofaidi huduma hii?
kitu kingine ambacho inabidi mwandishi aelewe ni kuwa kazi ya BBC siyo kuwa msemaji au tuseme PR wa serikali wala nchi ya Tanzania.
Mbona kilichoandikwa au kurushwa na BBC kilishatengezewa filamu inayozunguka nchi za ulaya!
kimsingi kama Tanzania inataka kupiga hatua kiasi cha kuwa na sifa nzuri tokana na kuwa na serikali mpya,inabidi ianze upya.
kwani kwa mfano hakuna mtu mzima mwenye akili asiyejua kuwa uwekezaji na ubinafsishaji karibu wote uliofanyika chini ya awamu ya tatu unanuka mazingira ya rushwa
huu ndiyo ukweli. au kwa vile walioripoti ni BBC basi inakuwa nongwa! mbona marehemu mwalimu Nyerere alishasema mazito kuliko haya! Mbona umma unashuhudia machafu kuliko haya!
je kwa mfano mtu akisema kuna mauaji ya vikongwe Tanzania atakuwa ameidhalilisha nchi/
Mtu akisema kuwa hata mgao wa umeme ni uzembe na h ujuma atakuwa anadhalilisha nchi? sasa tusemeje?
-
Comment #71
(Posted by jackline)
Rating
    
Ni vibaya sana. Hata kama ni kweli iko hivyo lakini wasinge onyesha hatharani namna hiyo.mimi niko Dernmark lakini sijaona kitu kama hicho.
-
Comment #72
(Posted by Graca)
Rating
    
Mataifa yaliyoendelea ndiyo vinara wa ukiukwaji wa haki za binadam. Iweje ya Africa ndiyo tu yanaongelewa.
Nimeisha USA kwa kipindi kirefu na nimona mengi, kiwango cha ukahaba, utumiaji wa madawa ya kulevya, ushoga, omba omba na ukiukwaji wa haki za binadam ndio utaratibu wa maisha. Hatujafikia hata nusu yake.
Ukiukwaji wa haki za binadam wanaofanyiwa waamerika weusi na watu wengine wenye asili ya Africa Marekani na Ulaya nadhani ndio ungefaa kuongelewa. Nimeona mtoto mdogo under 8 akitiwa pingu na polisi na kutupwa sero kisa kafanya utundu darasani? Hapa nani ni kinara wa ukiukwaji wa haki za binadam?
Tuwe makini na wachambuzi wa mambo badala ya kushabikia vitu kwa vile wameongea wazungu, huku ni kuwa brain washed.
Few isolated cases zinaweza kuwepo cha kushanga why dramatize them? Obvious there is a gain.
-
Comment #73
(Posted by Fikirini Ambuje)
Rating
    
Habari hii wengi tulioko nchini Tanzania tunaisikia tu watu wakisema na kusoma vipande vipande vya habari magazetini. Kwa ujumla wa yote habri hii ni msaada mkubwa kwetu kwani ni kama kumtoa mtu funza miguuni vinginevyo miguu itapinda. Pia wasawhili walisema hukuna uongo usiokuwa na ukweli ndani yake. Hivyo basi yaliyoyakweli tuyafanyie kazi, BBC labda wamesaidia kusema/kuonyesha lile ambalo hakuna Mtz ambaye angejitoa mhanga kwa hayo. Basi tujirekebishe, tuwatoe hao funza miguuni metu tusije tukashindwa kutembea. Hongera BBC.
-
Comment #74
(Posted by Amani)
Rating
    
Inasikitisha sana kusikia jinsi watanzania wanavyounga mkono kudhalilishwa kwa Taifa lao. Madhara ya kuonyeshwa kwa mambo mabaya kuhusu Taifa letu kwa mataifa ya nje haina nafuu yoyote kwetu zaidi ya kutudhalilisha kwa kila anaeona filamu kama hizo. Hakuna nchi duniani ambapo kila kitu kinachotendwa ni chema. Na wala hakuna nchi yeyote duniani ambapo hayo yanayotajwa kwenye filamu hiyo hayapo. Nadhani serikali inatakiwa kuchukua hatua za haraka kuhakikisha jina zuri la nchi yetu haliendelei kuchafuliwa na watu wetu wenye husda kama wakina Hubert Sauper. Kwanini turuhusu kutukanwa hadharani na tusichukue hatua yeyote? Kwanini watu hao wasionyeshe maovu kama hayo ambayo pia yapo kwenye nchi zao. Kwanini Tanzania tu. Ni faida gani wanazotaka kupata kwa kufanya hivyo? Sheria zitumike, na zitumike haraka iwezekanavyo. Sote tuna wajibu wakulinda heshima ya Taifa letu. Tusiwe vimbelembele kusifia ujinga wa watu wenye husda, ambao hata si watanzania.
-
Comment #75
(Posted by tracy)
Rating
    
Watanzania tunaoishi mwanza tunaiona hali halisi ya mapanki na pia ya watoto wa mitaani jinsi wanavyolala kwenye vibaraza na jinsi wanavyowaibia wananchi, hilo swala la machangudo pia lipo sema tuu kwa vile swala la uchangudoa ni la dunia nzima, lakini sisi wana MWANZA tumekuwa tukijiuliza kuwa hivi kweli serikali imeridhika na hawa watoto wa mitaani wanavyoteseka kweli??? watoto wadogo wenye umri chini ya miaka 12 kumi na mbili wavuta bangi wanafanya UFIRAUNI na watoto wadogo wa kike kuuza miili yao, hili ni jambo la kawaida kabisa hapa mwanza na kama hao wanaobisha kuwa mwanza hakuna mambo ya hivi na waje mwanza kwetu wajionee mambo haya ni ya kawaida kabisa na hakuna la uongo, labda hilo la silaha siwezi lisemea coz sijawahi ona. ila tunamuomba MH RAIS ajaribu kuwasaidia hawa watoto wamekuwa wakiishi maisha yasiyo faa kabisa. nina imani serikali ya awamu ya nne itatekeleza hayo.
-
Comment #76
(Posted by Nuru)
Rating
    
Hii ndio faida ya kuwakumbatia wageni na matokeo yake ni kuwachafua, hao wageni serikari yetu inayowakumbatia ndio hao hao ambao hawakuona mazuri ya Tanzania na wakaona mabaya tu ya tanzania na kwenda kuyaanika huko nchini kwao, NAJUA TANZANIA ITAJIFUNZA KUTOKANA NA MAKOSA.
-
Comment #77
(Posted by Pando)
Rating
    
Good report
-
Comment #78
(Posted by Said Rubbeya)
Rating
    
Kuhusu Minofu.
Hoja yangu ni kupinga udhalilishaji wa Watanzania na Waafrika kwa ujumla.
Ni suala la kweli kama wengi wanavyosema. Ukahaba upo. Silaha sina uhakika (Sijui km yupo mwenye uhakika kati yetu tunaochangia).Lakini hainifutii dhana kwamba huo ni UDHALILISHAJI na wengi wanaoona kwamba hakuna kujitetea juu ya Utanzania wetu na Uafrika wana hoja na sababu zao. Sababu zangu ni kama zifuatazo;- Nakubaliana na wanaolaani kitendo hicho cha kuidhalilisha Tanzania.Kama ni suala la Umaskini lipo wazi watu tunakula kila siku sawa na minofu hiyo mf. Samaki wakavu (perege,Kambare,papa,dagaa,nk). Suala la Ukahaba sababu ya Minofu hilo nalo halina mantiki.Ukahaba upo kila mahali na zaidi huko ulaya na kwingineko ambako hata leseni zinakatwa kwa ajili hiyo.Silaha za warusi? Hilo sijui kabisa.
Lakini fikiri juu umaskini kwingineko duniani? Fikiri juu Usenge, Ubasha, Usagaji uliopo Ulaya na America. Fikiri juu mazuri yaliyopo Afrika je yanaonyeshwa huko Ulaya? Fikiri juu ya Mabaya yaliyopo Ulaya na America Je yanaonyeshwa popote Duniani?Usafirishaji wa Silaha upo Afrika kuliko Ulaya na Amerika? Fikiri sana juu ya Utumwa maana yake,Uenezaji wake,Ujinga wetu wa kumezeshwa maneno na kuambiwa jinsi ya kuyatema!Ujinga wetu wa kupewa saa,kufundishwa kuitumia saa hiyo na halafu unapojaribu kusema ni saa ngapi wanakukatalia kwamba hivyo sivyo na kukumbusha kwamba wewe ni mjinga!!Fikiri juu ya kujitambua wewe binafsi, Je unafahamu thamani yako? Hatukuumbwa kwa rangi tofauti ili kuonyesha ubora wa mmoja wetu bali ni kwa nia ya kutambuana tu.Ni kweli Ulaya na Amerika wamewahi ktk maendeleo na ndio maana hakuna anaeruhusiwa kufika walipo kwani madhara yake wanayafahamu zaidi wao.Fikiri sana juu ya hilo.Kwa nini tunakwenda kuvuruga kila penye maendeleo duniani? Kila kitu duniani kinapangwa. Na watu makini duniani hupanga na kutekeleza.Baadhi wanasema hii si Siasa, si kweli, ukweli ni kwamba Siasa inaendesha maisha yetu kwa asilimia kubwa kuliko tunavyofikiri. Fikiri juu ya hilo,Kukueleza kwamba wewe ni Daktari,injinia,mhasibu,Mwanasheria, mwanahabari nk hiyo nayo ni siasa.TUSIJIDHALILISHE, TUSIKURUPUKE, .....Think about it!!!
-
Comment #79
(Posted by Madallein)
Rating
    
BBC wana la kutuambia, nasi tumelisikia, lakini nao lazima wawe wasikivu kama sisi. Yawezekana, mliyoyaona Mwanza ni ya kweli. Kama ada, Watanzania ni wepesi wa kujisahihisha, na naamini tutafanya hivyo. Ningetegemea kuwa kwa sasa BBC waone kuwa wana wajibu wa kuyafanyia kazi yale maeneo ambayo yanahatarisha kizazi hiki. Ningetegemea kuona BBC wanashirikiana na wanaharakati wengine ulimwenguni kuzinusuru nchi kama Tanzania ambazo BBC inafahamu fika jinsi mataifa makubwa yanavyozinyanyasa kwa umaskini wao. Angalia BBC kama mna macho, ni sumu ngapi sasa zinarundikwa katika nchi kama Tanzania, angalia uongo unaoenezwa kuhusu uhalali wa GMOs, tafiti hizo silaha hasa hasa zinatoka wapi kwa nanufaa ya nani. Huo uozo unaozungumziwa hapa ni kitu kidogo sana, kinachohitaji tu mwamko na kukirekebisha, na wala hakitaleta madhara makubwa kama mnavyotaka yawe. Fight issues that matter, Hizo hongo mnazozijua kuwa zinatumika na mataifa makubwa kuziangamiza nchi maskini, hayo ndio ya kuandika, hayo ndiyo ya kutumia gharama zote mnazotumia kuandika juu ya minofu ya samaki, andikeni yale yanayogusu uwepo wetu hapa duniani. Tumewasikia, tumeona aibu, lakini tukijirekebisha tunategemea na ninyi mtatumia raslimali zenu kutatua, kuelimisha na kuwafungua macho wale wote wanaoona kuwa ati minofu ni tatizo. Waone matatizo hasa ni nini. Hata hapo Uingereza yapo ya Mwanza. Tunayajua.
-
Comment #80
(Posted by h.kilawe)
Rating
    
Huyo muaandaji wa kipindi hizi alikuwa na agenda yake ya siri na nchi yetu Tanzania hiyo siyo desturi yetu hata kama hayo mambo yapo lakini kwa kiasi hicho mbona huko ulaya kuna ukahaba wa khali ya juu na hauonyeshwi.
Atafute kitu kingine hapo amekosa kazi ya kufanya By kilawa WA DSM.
-
Comment #81
(Posted by an unknown user)
Rating
    
huo ndio ukweli,pambaneni kuondoa huo uozo na si vinginevyo.picha aisemi uongo.
-
Comment #82
(Posted by an unknown user)
Rating
    
Huko London wanawake kibao wanajiuza mabarabarani sijui ni kipi cha ajabu BBC wameona mwanza.
-
Comment #83
(Posted by Diddy)
Rating
    
The writer of this article needs to go back to a journalism school. He has no freaking clue as to what he is supposed to be reporting as a journalist (if he is one!).
Anyway the truth of the matter is nothing seems to be fabricated in the BBC report. Somewhere somehow these things are happening in our country, the question is where is the leadership? where are the rules and regulations governing these things (or maybe we don't have them!!). One of your subscribers says she has seen even worse things in western countries. Well, I think he/she is missing the point. Just because people are using dope in the west, it doesn't mean that it is okay to do the same in our country. For anyone who has lived outside of our boarders, they can attest to the fact that our country is still very backwards in terms of law enforcement, business practice but we're very blessed to have Zombies in leadership positions, local and national.
Wake up Tanzania and start taking deliberate steps forward and clean up the squalor in our society.
-
Comment #84
(Posted by belarina)
Rating
    
Yeah, i concur with diddy, we are slowly being turned into a country of rabid xenophobes by a few journalists and have become increasingly intolerant about any negative image about ourselves as expressed by others, even if it is the gospel truth (remember the cartoon by a Tanzanian in the kenyan newspaper? Or the article from Kigali on EAC? How about Charles Onyango Obbo article in the East African?) We seem to be obsessed by a mistaken notion of superiority over others. It a high time we realise that so long as we are poor nobody cares what we think or whether we are a nation of angels or not. The world has now become a global village and issues touching on the environment or basic human rights transcend sovereign considerations tupende tusipende. We rant and rave amongst ourselves here and feel good and secure in our ignorant intellectual bliss not realising how archaic and outdated we actually appear. In the meantime it is THEM we want to point fingers at and blame for our own shortcomings.. Talk of the pot calling the kettle black! Sheeesh!!!
-
Comment #85
(Posted by jerry)
Rating
    
nchi yeyote inajisahihisha baada ya kusahihishwa, natumaini kwa upande wangu nawapongeza BBC kwa kuonyesha yale maovu ili tujisahihishe.
tuweke ulinzi wa kutosha katika viwanja vyetu vya ndege, tuwasaidie wanawake ili waache tabia hiyo ya kujiiuza ni shida na hali ya maisha kuwa ngumu. tuwaamasishe wazazi wawapeleke watoto wao shule ili wasijiingize kwenye ajira, lakini hiyo inatokana vilevile hali ngumu ya maisha.SERIKALI IJITAHIDI KUBORESHA MAISHA YA WANANCHI WAKE NA SIYO KUUZA MIGODI NK
-
Comment #86
(Posted by Alex Aggrey)
Rating
    
Hiyo ndiyo hali halisi. Swala sio kuitaka serikali ijibu hii kashfa, swala ni kuitaka serikali iondoe hiyo hali huko Mwanza na kwingineko ambako watanzania wanateseka na kunyanyasika. Kwa teknolojia iliyopo ni ujinga kufikiri kuwa tutaficha maovu yetu. Mwisho, kuna mambo mengine mabaya yanaendelea na tunafikiri ni ya kawaida hadi pale vyombo vya nje vitakapoonesha kidole. Hii yote ni kwa sababu tuna waandishi goigoi wavivu wa kufikiri. Rais Mkapa aliwajua vizuri waandishi wetu! Huyu wa sasa hivi mmh
-
Comment #87
(Posted by JOSEPHAT KAMUGISHA)
Rating
    
Before stop that broad cast, you need to know that story were true or not,then even if you want to keep the name of Tanzania, how do you to solve this problem which is already there Mwanzan Lets talk the trueth dont keep respection without consider human right in children and women,these busness men they wants to keep their status for their own befit but consider is it happening in Tanzania? or not then send this ideal to president
-
Comment #88
(Posted by Peter Mselewa)
Rating
    
Lets calls spade spade, our leaders did munch lots of public funds. What BBC expose was not fiction or invetions, its the reality of life in Tanzania. I believe that will act as a wake up call to our leaders and Tanzanians in general, more need to be done to improve the life, justice and workind condition of our people. As I did wrote to you guys before, we seems to be stuck in ujamaa eras where everything was ok in our eyes. Corrupt leaders were seems to be heros.Army Captains with no education back grounds were appointed as general managers of big factory like Fiberbords in Arusha.We should thanks BBC for expose that and accept critisism. Lets work on it now
-
Comment #89
(Posted by kazi)
Rating
    
The article has been either prepared without editting/proofreading or was typed by a tired and overworked person.There is a lot of misspelling.
Well researched and informative but poorly presented, a hitch that may cause a potential reader to shy away.
-
Comment #90
(Posted by Hemedi Begge)
Rating
    
Waheshimiwa wahusika wa suala hili sisi watanzania tunaoishi nnje ya Tanzania tumesikitishwa kwa kiwango kikubwa kuoneshwa kwa program hii kwani kumetudhalilisha kupita kiasi.Tanzania ni nchi tunayo jitahidi kuitangaza katika fani tunazo weza kadri ya uwezo wetu.Hii program italeta madhara kwa taifa letu lenye sifa nzuri hasa ya amani na ukarimu .nia ya hawa jamaa nikuipaka matope Tanzania tu sijingine zaidi ya hilo kwani kama nimaovu ya nchi yako mengi tu yanchi tofauti zinazokiuka haki ya binaadamu ikiweo hii uingerezayenyewe.wahusika tunaomba wachukue hatua za kisheria kulisimamisha suala hili hiiorogram ni kutuaka matope na kutuonea wivu wa kijasmii,amani,mshikamano tulio nao watanzania ndani hadi nnje ya Tanzania.Mungu ibariki Tanzania na watuwake.
-
Comment #91
(Posted by AMINAWAZIRIJUMARICHARDS)
Rating
    
aS SAD AS IT IS YET IT'S THE TRUTH,WELL WE TANZANIANZ MIGHT BE STILL A GROWING COUNTRY,HOWEVER WE NOT POOR, POVERY IS JUST AN STIGMA ATTACHED FOR THE MANY GREEDY TO PROFIT, I THINK THIS IS A TIME TO NAME AND SHAME THEM, AND IF THEY CONTINUE LET THE WORLD G8 AND UN AND CHARITIES STOP HELPING TANZANIA, BUT LET THEM VISIT AND HELP THE MANY SUFFERING AND VULNERABLE
-
Comment #92
(Posted by carer)
Rating
    
ni lini watanzania watajua kukubali ukweli. hata hapa ulaya tulipo kila siku tunaona vipindi vinavyoonyesha ni jinsi gani watoto wa hapa wanaotoka familia masikini serikali yao isivyowajali. sasa tanzania ni nchi masikini tunategemea kitu gani. baada ya kukaa ulaya kwa muda mrefu na kuifutalia siasa. kitu kimoja nilicho jifunza sisi watanzania atupendi ukweli. nikimahanisha tupo tayari kulala njaa kulikoni kusema jamani sina hela ya kula. na hiwapo hamna maendeleo bila ya mabadiliko. sito shangaa watanzania wakikataa kusikia ukweli wao lakini hawashangai kwanini wanaitwa masikini. mzungu anasema umaskini tabia namuunga mkono kwa hilo.
-
Comment #93
(Posted by carer)
Rating
    
ni lini watanzania watajua kukubali ukweli. hata hapa ulaya tulipo kila siku tunaona vipindi vinavyoonyesha ni jinsi gani watoto wa hapa wanaotoka familia masikini serikali yao isivyowajali. sasa tanzania ni nchi masikini tunategemea kitu gani. baada ya kukaa ulaya kwa muda mrefu na kuifutalia siasa. kitu kimoja nilicho jifunza sisi watanzania atupendi ukweli. nikimahanisha tupo tayari kulala njaa kulikoni kusema jamani sina hela ya kula. na hiwapo hamna maendeleo bila ya mabadiliko. sito shangaa watanzania wakikataa kusikia ukweli wao lakini hawashangai kwanini wanaitwa masikini. mzungu anasema umaskini tabia namuunga mkono kwa hilo.
-
Comment #94
(Posted by carer)
Rating
    
ni lini watanzania watajua kukubali ukweli. hata hapa ulaya tulipo kila siku tunaona vipindi vinavyoonyesha ni jinsi gani watoto wa hapa wanaotoka familia masikini serikali yao isivyowajali. sasa tanzania ni nchi masikini tunategemea kitu gani. baada ya kukaa ulaya kwa muda mrefu na kuifutalia siasa. kitu kimoja nilicho jifunza sisi watanzania atupendi ukweli. nikimahanisha tupo tayari kulala njaa kulikoni kusema jamani sina hela ya kula. na hiwapo hamna maendeleo bila ya mabadiliko. sito shangaa watanzania wakikataa kusikia ukweli wao lakini hawashangai kwanini wanaitwa masikini. mzungu anasema umaskini tabia namuunga mkono kwa hilo.
-
Comment #95
(Posted by mkereketwa)
Rating
    
UKWELI SIO KUZALILSIHWA BALI NDIO NJIA PEKEE YA KUTATUA MATATIZO, NIMECHOKA KUSOMA HABARI KUISIFIA HAMBAZO HAZINA UCHUNGUZI WOWOTE NA WALA HAZILETI MAENDELEO ILA KUFICHA MAOVU. HIVI NDIO WAANDISHI WA HABARI WA ULAYA WANAVYOFANYA KAZI KWA HIYO WATANZANIA JIFUNZENI
-
Comment #96
(Posted by Ngwesa)
Rating
    
uzuri wa watanzania ni kwamba sanyingine wanakubali ukweli lakini ikifikia utekelezaji- humwoni mtu! mpaka rais naye ana kula kona... kwamfano juzi katoa BILLION 1 mikoani za miradi ya maendeleo ambayo hakuna plan inayoonyesha jinsi fedha zitakavyotumika na kugawanywa in details, kazi hiyo waliachiwa mabenki ambayo tuyajua kuwa ni profit-seeking sikuhizi baada ya previtazation. so rais kaingia mitini baada ya kudamp fedha, mikoani wanashikana mashati ie Tanga pale. benki na wenyewe wanahakikisha wapata cha juu, who is accountable for development monies? hii BILLION 1 ingetakiwa kutolewa polepole hata kwa kipindi cha miaka miwili kuhakikisha kuwa hii miradi ni stable na accountability ipo! maendeleo huchukua muda na lazima watu hili walifahamu! sasa hizi BILLION moja moja zimefanya nini? kama sio UMASIKINI MAMBOLEO HUU!!!!!
-
Comment #97
(Posted by Bruno Denyutali)
Rating
    
It must be understood that the Western media has had always a systematic character assassination of our countries and the African Continent in general. Tanzania must be aggressive in information dissemination. It is not enough to silence BBC. It is important to show to the world the lies that the West has always perpetrated about Africa.
If one listens to BBC about President Robert Mugabe than one understands what BBC and the West in general is all about in Africa. They want an enslaved Africa not progressive Africa. They want to report wars in Africa not development. They want the AIDS in Africa not a vibrant Africa. They want a begging Africa not a Self reliant Africa. They want a poor Africa not a rich Africa.
History is however against the West. Today they face extinction as they have no people to replace them. We hope they will vanish as all liars have vanished in history.
-
Comment #98
(Posted by Bruno Denyutali)
Rating
    
It must be understood that the Western media has had always a systematic character assassination of our countries and the African Continent in general. Tanzania must be aggressive in information dissemination. It is not enough to silence BBC. It is important to show to the world the lies that the West has always perpetrated about Africa.
If one listens to BBC about President Robert Mugabe than one understands what BBC and the West in general is all about in Africa. They want an enslaved Africa not progressive Africa. They want to report wars in Africa not development. They want the AIDS in Africa not a vibrant Africa. They want a begging Africa not a Self reliant Africa. They want a poor Africa not a rich Africa.
History is however against the West. Today they face extinction as they have no people to replace them. We hope they will vanish as all liars have vanished in history.
-
Comment #99
(Posted by kubali)
Rating
    
KUBALI UBADILIKE, KAMA JAMBO NI KWELI SASA KWANINI KULIPINGA NA VIJISABABU VISIVYOKUWA NA MSINGI? KUBALI UBADILIKE TANZANIA, TUNATAKA UBADILIKE UMJALI MTANZANIA
-
Comment #100
(Posted by nchi yangu)
Rating
    
Kitu cha kufanya, ni kwenda mitaa mibaya na michafu ya Uingereza,kuchukua video na picha na kutangaza huko Afrika.Hawa hawana kitu, wana mitaa michafu na mibaya kulika hata ya huko nyumbani.Sheria ni "Jino Kwa Jino".Wanasema umalaya, wazungu wana umalaya mchafu sana!Nenda mitaani hapo, wazungu wengi wanatafuta wateja wa kiafrika.Tunaoishi nje, tunawajua vizuri sana!Pia,kama mchango, nashangaa kwa nini watu wanabatizwa majina ya kiingereza wakati tuna majina yetu wenyewe hata kama ni jina la mti!Unabatizwa jina ambalo hujui limetoka wapi huko kwenye vijiji vya uingereza? Ni vizuri kuwa kama waafrika wa Nigeria na Ethiopia, wana majina yao.Kwanza kwa nini Ziwa Victoria linaitwa hivyo? Wakati umefika kubadilisha majina na kutumia majina yetu,tulishatoka kwenye ukoloni zamani,ila bado tuna ukoloni wa majina!Tunaonekana kama vile hatuwezi kujenga majina yetu? Kisa, ukiwa na jina kama la Peter,then utaenda mbiguni kwa sababu St.Peter atakusaidia kumuonga Mungu.Wakati jina Peter kwa wakorintho au waebrania haliitwi hivyo!Badili majina,achana na maisha ya hao, na utamaduni wao.......
-
Comment #101
(Posted by nchi yangu)
Rating
    
Kitu cha kufanya, ni kwenda mitaa mibaya na michafu ya Uingereza,kuchukua video na picha na kutangaza huko Afrika.Hawa hawana kitu, wana mitaa michafu na mibaya kulika hata ya huko nyumbani.Sheria ni "Jino Kwa Jino".Wanasema umalaya, wazungu wana umalaya mchafu sana!Nenda mitaani hapo, wazungu wengi wanatafuta wateja wa kiafrika.Tunaoishi nje, tunawajua vizuri sana!Pia,kama mchango, nashangaa kwa nini watu wanabatizwa majina ya kiingereza wakati tuna majina yetu wenyewe hata kama ni jina la mti!Unabatizwa jina ambalo hujui limetoka wapi huko kwenye vijiji vya uingereza? Ni vizuri kuwa kama waafrika wa Nigeria na Ethiopia, wana majina yao.Kwanza kwa nini Ziwa Victoria linaitwa hivyo? Wakati umefika kubadilisha majina na kutumia majina yetu,tulishatoka kwenye ukoloni zamani,ila bado tuna ukoloni wa majina!Tunaonekana kama vile hatuwezi kujenga majina yetu? Kisa, ukiwa na jina kama la Peter,then utaenda mbiguni kwa sababu St.Peter atakusaidia kumuonga Mungu.Wakati jina Peter kwa wakorintho au waebrania haliitwi hivyo!Badili majina,achana na maisha ya hao, na utamaduni wao.......
-
Comment #102
(Posted by JM ORIGINAL,)
Rating
    
KWA NINI MNAONYESHA HIYO PICHA NYIE INAWAHUSU NINI, ACHENI USENGE, MNAKUWA KAMA MNAGONGWA. MAFARA NYIE, NYIE MBONA MNATOMBWA TOMBWA HOVYO ATUSEMI, KWANZA NYIE NDIO MALAYA WA KUTUPWA. MNAFIRALA KILA SIKU NA MNATAKA KUANZISHA SHERIA HILI MUENDELEE KUFILANA. MAFALA NYIE. KUMA ZENU ZINANUKA. NA MBOO ZENU NDOGO.
-
Comment #103
(Posted by Lanyo)
Rating
    
Ningependa tu kuwashauri Watanzania wenzangu kuwa tuwe makini na uchambuzi na wachambuzi wa mambo badala ya kushabikia vitu kwa vile vimeongewa au kufanywa na mtu fulani, Tuwe wahalisia (objective and not subjective). Swali langu kwetu ni je mambo hayo yapo kwetu Mwanza? Je, lengo la BBC ni nini: kutusaidia kuona matatizo yetu ili tutafute ufumbuzi au kutudhalilisha kama wengi wetu tusemavyo? swali la mwisho: Je toka tulipoona na kusikia hali yetu huko mwanza, tumechukua hatua yoyote, yaani hali imebadilika au kubadilishwa? Tukiwemo Mwanza leo, hatutaona na kushuhudia hali hiyo ya vichwa vya samaki na masubi yake, watoto kufanyishwa kazi, ukahaba, kinyesi na mazingira machafu?
Kama mambo hayo bado yapo, basi elimu ya bure haina maana wala faida. Kama tumeelimika, tukastaarabika, basi sisi ni waadilifu.
Je, kama serikali tumefanya chochote au porojo tu za vyombo vya habari za sikio la kufa halisii dawa?
Picha zilizochukuliwa ni mbaya, lakini uhalisia ambako picha zimechukuliwa ni mbaya zaidi. Je ni kweli? Fikiria tena mara mbili.
-
Comment #104
(Posted by Cyprianernest@yahoo.com)
Rating
    
Mimi hilo niliwahi sikia kwenye BBC-swahili.Lakini hata kama ni ukweli inabidi umwambie mtu ajirekebishe na wala si kwenda kwa mtu mwingine na kumwambia habari za fulani.Huo utakuwa ni unafiki na siku zote haujengi.Mimi hilo ni kosa kwa BBC kwa sababu uchumi,nakshi na raha ya nchi yetu inapungua.Sio kila habari itangazwe,Mwalimu Nyerere alisema
-
Comment #105
(Posted by mrs hans .)
Rating
    
kwanza ninamshukuru rais wetu kufanya juu chini kuitangaza nchi yetu ktk nchi zilizoendelea.lakini ndugu zangu watanzania kwenye ukweli lazima tuseme ukwelini ni kwamba nchi yetu ni nzuri ila kweli hivyo vitu vinafanyika.hivyo msiilaum BBC kwani imetusaidia sisi wa hali chini.hao wanao lalamika wao ndio wanaokula hela ya serikali.ndio maana wanajifanya kuilalamikia BBC.tchaoooooooooo
-
Comment #106
(Posted by rehema)
Rating
    
nikiwa kama mwanasheria mtarajiwa ambaye sas ninasoma kwenye nchi za wenzetu walioendelea ndugu zangu watanzania tuamke kwani.ninaipongeza sana BBC kwa kueleza ukweli wa tanzania hivyo nyie mnaye kula hela ya tanzania msijifanye kwamba hivyo vitu havipo vipo ndio maana vimeelezwa.chakufanya muibadilishe tanzania mtaona kama BBC itaezeza vitu kama hivyo vipo ndio maana vimesemwa.msipende kulalamika wakati kiyu ni ukweli kuweni wakweli kama BBC.
-
Comment #107
(Posted by twilumba)
Rating
    
kwakweli serikali ya tanzania inashangaza sana kwani kila siku hii serikali inapewa misaada ya kusaidia wananchi wake especially kwa lengo la kuiendeleza nchi hiyo misaada inaishia hewani pia tunachojua kuambiwa tumepewa misaada na wala hatuambiwi hiyo misaada imefanya nini na wapi.misaada hiyo inawanufaisha wenye hela nikimaanisha serikali MUNGU waamushe wananchi wa tanzania wajue haki zao.kwa kweli ninaipongeza sana BBC kwakueleza ukweli wa nchi ya tanzania hivyo ndivyo watu wa tanzania wanavyoonewa na ambavyo hawapewi haki za kimsingi.kinachotakiwa watanzania wenzangu tuwe wakweli kama BBC. BBC imeeleza ukweli wa tanzania pia imetusaidia sisi wanyonge tunaoonewa kila siku.MUNGU WASAIDIE WANANCHI WA TANZANIA TENA WALE MASIKINI SIKU WAJE WAWE MATAJIRI KAMA HAO WANAOKULA HELA YA SERIKALI YA TANZANIA.WATANZANIA TUAMKENI JAMANI KWANI NCHI YETU NI NZURI SANA KWANI INAMALI NYINGI SANA INASHANGAZA KUONEKANA NCHI YETU IKO KWENYE KUNDI LA NCHI ZA AFRIKA MASIKINI HII NI AIBU.BBC endeleeni kueleza ukweli wa tanzania na wala msiache kabisa mpaka itakavyo badilika.have nice day BBC.
-
Comment #108
(Posted by Molloi)
Rating
    
SASA BBC WAMEANIKA HAYO YOTE ILI WATUSAIDIE AU UCHOCHEZI TU? TAHADHARI
-
Comment #109
(Posted by Augustine Mhando)
Rating
    
Napenda kuchangia maoni yangu kama ifuatavyo kwenye maisha ya kila siku kuna mazuri na mabaya na inabidi tukubali yote.
Swala la kusema tusikubali wasionyeshe kipindi kama hicho hiyo ni kukiuka taaluma ya waandishi wa habari na vyombo vya television.
Nafamu kuonyesha picha kama hizo ni aibu kwa taifa lakini tujiulize wenyewe kwamba kilicho onyeshwa ni kweli au wanataka kupaka matope nchi yetu.Kama sikweli tunabidi tupigane kutumia nguvu za hoja kukanusha swala hilo vikali sana. Lakini kama ni kweli ni wajibu wa serikali na kila mzazi na wananchi wote kwa ujumla kukemea swala la watoto wadogo kufanyishwa kazi na pia kukemea swala la Tanzania kutumika kupitishia silaha ambazo kwa upande mmoja kama ni kweli zinakwenda kuua ndugu zetu wenyewe na mara nyingi kutugeukia sisi wenyewe pale zinapokwenda kwenye mikono ya majambazi.
Mimi ni Mtanzania na nimekaa kipindi kirefu cha maisha yangu Tanzania na kuna mambo mengi yanafanyika na Serikali yetu inafahamu na inafumbia macho,njia sahihi ni kwa watu ambao wanauchungu kurusha hewani ila dunia ifahamu ukweli japo kuwa tunaaibika lakini kwa muono wangu hiyo ndio njia sahihi kwa serikali kujifunza na kutafuta njia muafaka kuondokana na mambo yote maovu kama wizi wa mitihani,Rushwa za wazi, Upendeleo makazini na masomoni, Matibabu,ubabaishaji wa usafiri wetu ambao ni hatari kwa wananchi na mambo mengine mengi.
Tuwe wawazi wa kukubali mazuri ambayo Juma pinto na mwenzake Abubakari Faraji wanafanya kwenye Sky London,Uk. na pia tukubali pale tunapokosolewa kwani hiyo ndio jia muafaka ya kujifunza na kujirekebisha,Inabidi tukumbuke 'Rome is not build in One Day'It takes ages to builds and still up to now they keep building
-
Comment #110
(Posted by mtwange)
Rating
    
upande wa lugha baadhi ya maneno si sahihi
-
Comment #111
(Posted by Jay4)
Rating
    
Ukweli unauma,hayo mambo yote yapo bongo,ngoja tujionee aibu sasa.Hongera BBC,ka nchi kameoza,mijikashfa nyomi,hivyo vichwa vya samaki vinaliwa sana na walala hoi,minofu inaenda ulaya,stupid.
-
Comment #112
(Posted by an unknown user)
Rating
    
NENO MAPANKI HALIKUANZISHWA NA MTENGENEZAJI WA FILAMU HIYO, YEYE ALIKUTA WATU WA MWANZA WAKITUMIA HAYO MABAKI AMBAYO WAO WANAYAITA MAPANKI. HUO NDIO UKWELI, SASA HIVI SOKO LA FERI DAR PIA YAPO MAPANKI.HAPA NI KARIBU KABIA YA IKULU.JAMBO JEMA LABDA WAKAMATWE WANAOKULA HAYO MAPANKI KWA KULITA AIBU TAIFA.
-
Comment #113
(Posted by ester)
Rating
    
Hii article imeongelea vitu vingi mno vya nchi yetu mimi nakubali kuwa vingi ni ukweli maana kila nchi ina mazuri na mabaya yake. haya ni mabaya yetu sasa je hiyo filamu ilitengenezwa kwaajili yakwenda kuonyeshwa nchi za nje au ilitengenezwa kwa ajili yanani? katika nchi lazma tutofautiane kuna wenye hali za juu na wenye hali za chini, swali nini lengo la hiyo filamu?? hiyo filamu imetumika vibaya sana chukueni hatua jamani......
-
Comment #114
(Posted by mzalendo kamili)
Rating
    
ile ilikuwa si kudhalilisha nchi bali ilikuwa ni njia moja wapo ya kutufungua macho hata sisi wananchi amboa tuko mbali, na wale ambao hajui ni lipi linalo endelea nchini.kwa upande fulani niliudhunika kama raia wa tanzania kuona nchi yangu ikitumiwa kama 'base' ya kushushia siraha zinazo waumiza majerani zetu, nchi kama congo, rwanda, uganda, burundi nk. SASA ukweli unajulikana serikali inabidi ijue kuwa tunajua.. tunataka ulinzi makali pale mwanza, na tunataka ile minofu ya samaki ibaki pale mwanza na sio mifupa ya samaki. pesa za hizo samaki zinaenda wapi na mbona wananchi wanaoishi karibu na hilo ziwa victoria hawana chochote wanachofaidika nacho, god bless TANZANIA na watu wake, mzalendo kamili(netherlands)
-
Comment #115
(Posted by humph)
Rating
    
watu wengine kudharau kwenu ndio asili yenu kama kweli mmeingalia hiyo documentary ki uhalisi hamuwezi kusema ni ukweli thats was biashara...hiyo tabia yenu ya kudharau kwenu ndio inawafanya muwe watumwa uku ulaya mpaka kufa kwenu,,,na mtapiga sana deki kwa elimu zenu fake.
-
Comment #116
(Posted by Richard)
Rating
    
kama kuna ukweli unaosemekana na jamaa wa BBC basi hakuna haja ya kulalamika,bali ni watu wanatakiwa kuacha tabia hizo mbaya za kujiuza,siokwamba wote wanapenda kujiuza bali ni umasikini tulionao sisi watanzania,ijapokuwa tunayo rasilimali zote,ambazo zinamilikiwa na watu wachache wenye mabavu,hivyo serikali wanatakiwa kulingana na kuona maasi yalioonyeshwa na BBC watafute njia ya kuwasaidia hao wanaojiuza maana kitu kinachochangia kufanyika kwa maasi hayo ni umasikini mkubwa uliopo nchini,
na vilevile kuna uwezekano wa baadhi ya viongozi kukubaliana na BBC kurusha kipindi hicho ili waweze kupata misaada na wapate kuweka hiyo misaada mifukoni mwao maana ndivyo hali halisi ya viongozi wetu maana wana njaa sana na ni wabinafsi.
Jamani ushauri wangu ni kwamba tufumbue macho maana hakuna kitu kinachofanyika serikali isijue wananchi tutapiga kelele lakini uzi ni uleule,kinachotakiwa ni kukaa chini wenyewe na kutafuta namna ya kuondokana na umasikini na tusitegemee sana misaada maana ndiyo inayozilemeza nchi nyingi za Afrika kwani tunasubiri misaada badala ya kutumia rasilimali tulizonazo ndugu zangu.
Na vilevile serikali iwajibike kuwasaidia wananchi wasiojiweza na ili kuweza kupunguza umasikini tulionao watanzania maana ndio unaochangia kuongezeka kwa ugonjwa wa ukimwi kwa kasi zaidi.
Na vilevile serikali inapoletewa misaada ihakikishe inawafikia walengwa maana hata wakijilundikia hizo pesa haziwafikishi popote wataziacha hapahapa duniani ni bora ziwafikie walengwa ili angalau kupunguza umasikini uliokithiri nchini
-
Comment #117
(Posted by suleiman)
Rating
    
Samahanini kama nyinyi hamtaki kuamini basi
hatasisi ujerumani kimesha oneshwa
na tunaamini hayo.
hiyo nchi ni ya kibinafsi,usi lalelale si kipofu wewe hayo uliyoyaona ndiyo,siku ya mwisho wewe nishahidi.
usi pende,yasiyo ya haki,au utafufuliwa kipofu.ahsante sana.
-
Comment #118
(Posted by suleiman)
Rating
    
Huwo si uzushi bali hata sisi ujerumani
tumekiona hicho{docu}kama hamtaki kuamini
ni nyinyi na imani zenu
tunataka haki kubali,sidhani kuwa etii BBC
inaiyonea choyo SKY kufikiria ufinyo etii
huyu huonesha vipindi kuhusu tz ndio BBC inaonesha sifa,mazingira mabaya,laa nimakosa ya kutofahamu madhumuni ya kufanya hivyo,BBC imefichua maovu ya siri
Hivyo ndivyo hali ilivyo,hakuna kupiga kelele mmewachagua wenyewe,majini ya tutafunayo ndiyo hayohayo,humaliza badhi ya femily.hao walio onyesha na kukufunamacho MMungu awape uwezo kutufunulia mengine amin
Submit Comment
|
|
Your Favorite Articles
|
|
View All Favorites
|
|
|