Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mkuu wa mkoa akiri kukabiliwa hali mbaya kielimu
Mkuu wa mkoa akiri kukabiliwa hali mbaya kielimu
By Habari Tanzania | Published  01/19/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Samuel Msuya, Morogoro

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Meja Jenerali Mstaafu, Said Kalembo amekiri kuwa hali ya elimu mkoani kwake ni mbaya, na kuwahimiza madiwani kuwahamasisha wananchi kukamilisha ujenzi wa madarasa ya shule za sekondari kabla ya machi 15, mwaka huu.

Kauli ya mkuu wa mkoa imetolewa siku chache baada ya kumuahidi Waziri Mkuu, Edward Lowassa kuwa mkoa utakamilisha ujenzi wa madarasa ifikapo Machi 15, ili kuwawezesha watoto wote waliofaulu mtihani wa darasa la saba mwaka jana kupata nafasi ya kujiunga kidato cha nne

Wito huo ulitolewa jana mjini hapa katika kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, ambapo alisisitiza kuwa viongozi wote kuanzia ngazi ya wenyeviti wa vijiji, watendaji, waratibu wa kata na madiwani wawajibike kufanya kazi hiyo.

Amewataka viongozi hao kuwa na uchungu na elimu huku akisisitiza kwamba, madiwani wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha kuwa ujenzi wa sekondari za kata unakamilika kabla ya Machi 13.

Awali Meya wa manispaa hiyo, Profesa Romanus Ishengoma, alisema katika kukabiliana na jambo hilo, manispaa yake hadi kufikia Machi 15 itakuwa imeshakamilisha ujenzi wa shule nne za sekondari.

Profesa Ishengoma alisema mbali na kukamilisha shule hizo nne pia manispaa hiyo inatarajia kuongeza mikondo katika shule zake nane za sekondari, ili ziweze kuwachukua wanafunzi hao waliokosa nafasi kutokana na uhaba wa madarasa.

Aliongeza kuwa manispaa hiyo kwa sasa imeweka kipaumbele katika ujenzi wa shule hizo na kwamba, imesimamisha masuala mengine ili kufanikisha utekelezaji huo.

Meya huyo aliongeza kuwa endapo mipango hiyo itakamilika kwa wakati, manispaa hiyo itakuwa na uwezo wa kuchukua asilimia 77 ya watoto waliofaulu badala ya asilimia 70 ya awali


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.