Na Stephano Simbeye, Mbozi
WASAFIRI 150 na magari kadhaa yakiwemo ya abiria na mizigo yamekwama katika eneo la Miangarua katika barabara ya Tunduma – Sumbawanga baada ya barabara hiyo kuharibika kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha hivi sasa.
Baadhi ya madereva walimwambia mwandishi wa habari hizi kuwa iwapo serikali haitafanya matengenezo ya dharura kuna uwezekano mkubwa wa barabara hiyo kufungwa.
Dereva Elieza Mkisi wa gari la Mamlaka ya Hali ya Hewa alisema alilazimika kupitia porini kwa kuwa gari lake lina nguvu, lakini alisikitishwa na kukwama kwa mabasi mawili ya Summry yaliyokuwa na abiria zaidi ya 150.
Naye Mshamu Abdu, dereva wa lori lenye namba za usajili T413 AGY alieleza kuwa tatizo hilo lisipopatiwa ufumbuzi mapema kuna uwezekano bei za bidhaa na nauli kupanda kufuatia ubovu huo wa barabara hiyo.
Akina mama na watoto ndiyo walioathirika zaidi kutokana na kukwama kwa mabasi hayo kwa kuwa hakubeba vyakula kwa kuamini kuwa masaa matatu hadi manne yangetosha kumaliza safari.
Meneja wa Wakala wa Barabara (Tanroads) Mkoa wa Rukwa hakuweza kupatikana ili kutoa ufafanuzi juu ya hatua zitazokazochukuliwa