Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Daladala zasusa!
Daladala zasusa!
By Habari Tanzania | Published  06/13/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Mabasi yanayosafirisha abiria Jijini almaarufu kama daladala yamekisusa kituo cha mabasi cha Makumbusho na kukiacha cheupee na tope lake utadhani kimetifuliwa na tinga tinga.

Kufuatia hali hiyo, daladala zililazimika kupita mitaani kusanya abiria.
Mwandishi wa habari hizi aliyefika kituoni hapo mapema leo amekuta kituo kikiwa kitupu bila abiria wala daladala.

Baadhi ya abiria waliozungumza na Alasiri wamesema kituo hicho kwa sasa hakifiki kutokana na kutapakaa matope kila sehemu na kufanya abiria ’walioulamba’ kula tope hadi magotini.

Mwandishi ameshuhudia baadhi ya daladala zikipita mitaani kukusanya abiria katika makazi ya watu na zingine zikilazimika kurejea katika kituo cha zamani cha Mwenge kusaka abiria.

John Martin mkazi wa Makumbusho amesema maamuzi ya uongozi wa Jiji la Dar es Salaam kukihamishia kituo cha Mwenge katika eneo hilo kabla hakijakamilika ni ubabaishaji.

’’Kituo hiki ni cha kisasa na kimejengwa kwa gharama kubwa, lakini cha kushangaza kimefurika matope na hakifai tena’’ amesema Martini.

Baadhi ya abiria waliodamkia kituoni hapo walionekana wakihaha baada ya kukuta kituo ’kimeyeyuka’.

Hali hiyo ilizua tafrani baada ya abiria hao kukosa mwelekeo na wasijue wapate wapi usafiri wa kuwahi makazini mwao.

’’Jamani nimejitahidi kutembea kwa miguu mpaka huku halafu nakuta hakuna usafiri, sasa tukapandie wapi magari au tutembee mpaka Moroko’’, mama mmoja ambaye hakutaja jina lake alisikika akilalamika.

Kero hiyo ya tope hata hivyo imekuwa neema kwa wajanja wachache ambao wameibuka na mradi mpya wa kusafisha miguu ya watu iliyojaa tope kwa gharama ya shilingi 100 kwa kila anayehudumiwa

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.