Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  TABORA YAFUNGWA SETI 3-0
TABORA YAFUNGWA SETI 3-0
By Prosper Kwigize | Published  01/8/2007 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na. Prosper Kwigize (0754 077478)
Tabora
 
Timu ya mpira wa wavu ya mkoa wa Tabora ilishindwa kabisa kuonesha makucha yake kwa timu ya wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma baada ya kufungwa jumla ya seti tatu kwa sifuri katika mpambano wa kirafiki kati ya mkoa wa Kigoma na Tabora.
 
Kipute hicho cha aina yake na cha nguvu kilichezwa jumamosi iliyopita katika uwanja wa muungano mesi unaomilikiwa na jeshi la ulinzi wa Tanzania JWTZ mjini Tabora baada ya timu ya Tabora kutoa mwaliko kwa timu ya kibondo.
 
Ikiwa chini ya nahodha wake mahili Bw. Isaya Nzuguru Kibondo Volleyball Club- KVC inayoundwa na vichana wadogo chini ya miaka 23 ambao pia hucheza soka katika moja ya vilabu vya wilaya ya Kibondo, waliongoza mwanzo hadi mwisho wa mpambano huo dhidi ya Tabora.
 
Wakicheza mbele ya kaimu mkuu wa mkoa wa Tabora Bw. Moshi Mussa Chang’a ambaye ni mkuu wa wilaya ya Tabora, vijana wa timu ya Tabora walijikuta wakiambulia nusu ya point katika kila mchezo kwa kushindwa na wababe wao waliopata point 25 kila mzunguko.
 
Katika mzunguko wa kwanza (round) timu ya Kibondo ilishinda kwa jumla ya point 25 dhidi ya 19 za Tabora na mzunguko wa pili tabora ilizidiwa zaidi kwa kufungwa jumala ya point 25 kwa 16.
 
Mzunguko wa mwisho ambao ndio uliowapa ushindi Kibondo uliwaacha hoi zaidi wenyeji wao baada ya kujikuta wakiambulia point 11 kwa 25 na hivyo mwamzi wa mpambano huo Bw. Herbert Ntibakazi kuitangaza Kibondo kama mshindi wa mpambano huo kwa seti 3-0.
 
Aibu hiyo kwa wenyeji Tabora ilishuhudiwa pia na meya wa Manispaa ya Tabora mheshimiwa Peter Lembeli na mkuu wa brigedi ya jeshi kanda ya Tabora Luteni kanali Methew  Sukambi ambao walionesha wazi kufurahishwa na vijana wa Kibondo kichezo.
 
Akitoa mawaidha baada ya mchezo huo kaimu mkuu wa mkoa wa Tabora Bw. Chang’a amewapongeza sana Kibondo kwa kuonesha kwamba walikuwa na maandalizi pamoja na mshikamao miongoni mwao na katika mchezo pia.
 
Aidha ametoa wito kwa mkoa wa Tabora kuanza mara moja mazoezi ya michezo mbali mbali ili kuondoa aibu ambayo imekuwa ikiukuta mkoa kimichezo hasa wanapopambana na mkoa wa Kigoma .
 
Mkoa wa Kigoma umekuwa ukiwashinda majirani zao wa Tabora katika michezo mbalimbali na katika kombe la Taifa Kigoma iliuondoa mkoa wa Tabora katika mechi zote mbili kwa ushindi wa 2-1 na 2-0

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.