Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Hofu ya kimbunga yatanda Dar
Hofu ya kimbunga yatanda Dar
By Habari Tanzania | Published  12/24/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:
na Dauson Harold

WANANCHI wa Mkoa wa Dar es Salaam wametahadharishwa juu ya uwezekano wa kutokea kwa kimbunga kitakachoambatana na mvua na upepo mkali.

Tahadhari hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Alfred Tibaigana, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana.

Kamishna Tibaigana alisema taarifa iliyotolewa na Idara ya Hali ya Hewa nchini imetahadharisha kutokea kwa kimbuga hicho.

Tibaigana alisema wananchi wanapaswa kuwa makini na taarifa za uwezekano wa kutokea kwa kimbunga hicho kwa kuepuka kuogelea baharini hasa kutika kipindi hiki cha Sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya.

Alisema Polisi wataweka ulinzi katika maeneo ya ufukwe wa bahari ambapo askari wa doria watakuwapo katika maeneo hayo ili kuhakikisha hali ya usalama inakuwapo.

Aidha Tibaigana alisema kutokana na hali ya wasiwasi ya ubora wa kivuko kinachosafirisha abiria kutoka Magogoni kwenda Kigamboni, watumiaji wa kivuko hicho, wametakiwa kipindi hiki cha sikukuu, kutojazana katika kivuko ili kuepuka uwezekano wa kivuko kuzidiwa na kusababisha ajali

Aliwataka watumishi wa kivuko hicho kuwa makini na kutoa taarifa kila mara kinapokwama au kupata tatizo jingine lolote.

Alisema watumishi wa kivuko hicho wanapaswa kuhakikisha kuwa hakijazi abiria kupita kiasi na madereva wanaopenda kwenda Kigamboni kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Krismasi watumie njia ya Kongowe badala ya kulazimisha magari kupitia katika kivuko hicho.

Tibaigana alisema amewaelekeza makamanda wa Polisi wa mikoa, wilaya na vituo kufanya tathmini ya makanisa ambayo yatakuwa na ibada za usiku ili yapewe ulinzi.

Alisema familia zitakazokwenda kushiriki ibada usiku, zihakikishe kuna ulinzi katika nyumba zao na polisi watafanya doria za jumla mtaani.

Kwa wenye magari ambao watayatumia kwenda nayo kanisani, alisema hawataruhusiwa kuyaondoa mpaka ibada itakapomalizika na kwamba atakayekiuka agizo hilo atachukuliwa hatua za kisheria.

Alisema ufyatuaji wa fataki hautaruhusiwa katika kipindi chote cha sikukuu za Krismasi na mwaka mpya kutokana na kujitokeza kwa vitendo vya uhalifu wa kutumia silaha.

Alisema yeyote atakaye kuwa na mtoto na kumwacha kupotea atachukuliwa hatua za kisheria, alisema askari hasa wa kike watakuwa katika maeneo watakayokuwa wakisherehekea watoto.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by Aichi)
    Rating
    The artile is so good,it make a good summary for someone to get a clear picture even if you did not have any idea of what is going on.
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.