Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Tido Mkurugenzi Mtendaji TUT
Tido Mkurugenzi Mtendaji TUT
By Habari Tanzania | Published  12/20/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mwandishi Wetu
 
RAIS Jakaya Kikwete amemteua Dunstan Tido Mhando, kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utangazaji Tanzania (TUT).
 
Kwa mujibu wa kituo cha televisheni cha Channel Ten cha Dar es Salaam, kiliikariri Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo kuwa Tido anachukua nafasi ya Samwilu Mwaffisi.
 
Taarifa hiyo ilisema uteuzi huo umeanza Desemba 16, mwaka huu. Kabla ya uteuzi huo Tido alikuwa Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).
 
Akizungumza katika kipindi cha Dira ya Dunia cha BBC jana jioni, Tido alithibitisha kwamba ameteuliwa kuongoza Taasisi ya Utangazaji Tanzania.
 
Tido aliwashukuru wafanyakazi wa BBC kwa ushirikiano waliompa wakati wa uongozi wake wa miaka saba, akiwa Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC na miaka mingine kadhaa akiwa mtumishi wa kawaida wa shirika hilo.
 
Alisema ana matumaini kwamba atapata ushirikiano kutoka kwa wafanyakazi wenzake wa TUT kwa kuwa wengi wao alishafanya nao kazi alipokuwa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD), ambapo alianzia kazi miaka ya mwisho ya 1960.
 
Baada ya kuondoka RTD Tido alijiunga na Sauti ya Amerika (VOA), kituo cha Nairobi nchini Kenya na baadaye alijiunga na BBC.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.