Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  JK atimiza mwaka
JK atimiza mwaka
By Habari Tanzania | Published  12/21/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mwandishi Wetu
 
RAIS Jakaya Kikwete jana ametimiza mwaka mmoja wa uongozi wake madarakani na leo atazungumza na makundi mbalimbali ya jamii katika kuelezea mafanikio na changamoto za serikali yake ya awamu ya nne.
 
Kwa mujibu wa Mwandishi Msaidizi wa Rais, Maura Mwingira, Rais Kikwete ambaye yuko Dodoma kikazi ataadhimisha kutumiza mwaka mmoja wa uongozi wake kwa kuzungumza na vikundi vya jamii mjini Dodoma.
 
Alisema hotuba ya Rais Kikwete itatangazwa moja kwa moja na Televisheni ya Taifa na Radio Tanzania Dar es Salaam.
 
Rais Kikwete alichaguliwa kwa kura za kishindo kwenye uchaguzi uliofanyika Desemba 14, 2005, na aliapishwa Desemba 21, 2005 katika sherehe zilizofanyika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
 
Serikali ya Rais Kikwete ina baraza la mawaziri 29 na naibu mawaziri 31 ambao aliwateua Januari 4, mwaka huu na aliwapishwa Januari 5, mwaka huu.
 
Waziri Mkuu Edward Lowassa aliteuliwa Desemba 29, 2005 na kupitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano siku hiyo hiyo na aliapishwa rasmi Desemba 30, 2005 katika sherehe zilizofanyika Ikulu ya Chimwaga, Dodoma.
 
Rais Kikwete mara baada ya kuliapisha baraza lake la mawaziri alifanya ziara katika kila wizara kwa lengo la kujifunza na kueleza matarajio yake ya kiutendaji katika wizara hizo.
 
Kipindi cha mwaka mmoja Rais Kikwete amekwisha fanya mabadiliko ya baraza la mawaziri Oktoba , mwaka huu kwa kuwabadilisha wizara baadhi ya mawaziri na naibu mawaziri.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.