Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Akukweti kupelekwa nchini Afrika Kusini
Akukweti kupelekwa nchini Afrika Kusini
By Habari Tanzania | Published  12/20/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mwandishi Wetu

MADAKTARI wanaomtibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Maafa), Juma Akukweti, aliyepata ajali ya ndege mjini Mbeya, wamesema anapaswa kupelekwa nchini Afrika Kusini, kwa matibabu maalumu ya majeraha ya moto.

Wamesema Akukweti anahitaji kupatiwa matibabu maalumu ambayo hayawezi kutolewa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Wakizungumza na Waziri Mkuu, Edward Lowassa, jana aliyekwenda kumjulia hali, madaktari hao walisema wamefanikiwa kumfanyia upasuaji katika mkono wake wa kushoto ulioungua.

Walisema wameshindwa kumfanyia upasuaji kwenye mguu ulioungua kwa sababu bado kuna majereha ya moto, ambayo yanahitaji tiba maalumu ambayo haipatikani katika Hospitali ya Muhimbili.

Lowassa ambaye alitaka kujua kama tiba hiyo inahitajika kwa majeruhi wengine, walimwambia kuwa hali za majeruhi wawili zinaendelea vizuri na hawahitaji kupelekwa Afrika Kusini.

Walisema majeruhi mwingine, George Bendera, ambaye amelazwa katika chumba cha uangalizi maalumu (ICU), hawezi kusafirishwa kwa sababu hali yake si nzuri.

Pamoja na Waziri Akukweti, majeruhi wengine ni msaidizi wake, Nestas Kanje na rubani wa ndege hiyo ya Tanzanair, Martin Sumari.

Naye Mwandishi Wetu, Magreth Kinabo, anaripoti kuwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utawala Bora, Philip Marmo, jana aliiwakilisha serikali kwenye mazishi ya Mkuu wa Mradi wa Uendelezaji Masoko kwa Wakulima (MSDP), Nathaniel Katinila.

Marehemu Katinila ni mmoja wa waliokuwa wamejeruhiwa katika ajali ya ndege iliyotokea mjini Mbeya, Jumapili iliyopita.

Akizungumza baada ya mazishi hayo, Marmo alisema serikali imempoteza mtumishi aliyekuwa na bidii ya kazi.

“Kazi alizozifanya marehemu ni matunda ya kujivunia, kwani alikuwa mchapakazi hodari,” alisema Marmo.

Alisema marehemu alipata mafunzo mbalimbali ya uchumi wa kilimo na uongozi ndani na nje ya nchi.

Marehemu Katinila aliajiriwa na serikali mwaka 1984, ameacha mke na watoto watatu, wawili wa kiume na mmoja wa kike.

Ibada ya mazishi yake iliongozwa na Askofu Steven Mollel wa Kanisa la Pentekoste Arusha, ambaye alisema marehemu alitumia muda wake pia kwenye shughuli za kanisa.

Alizikwa jirani na kaburi la Theresia Nyantori, mwandishi wa Idara ya Habari (MAELEZO), ambaye pia alifariki dunia katika ajali ya ndege hiyo, kwenye makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.