Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Denmark yaichapa kiboko Tanzania
Denmark yaichapa kiboko Tanzania
By Habari Tanzania | Published  12/14/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mwandishi Wetu

DENMARK imesema itapunguza Sh4.1 bilioni sawa na asilimia 20 ya fedha za msaada katika bajeti kuu ya Tanzania mwakani, baada ya serikali kushindwa kutimiza ahadi yake ya kupeleka bungeni muswada wa sheria mpya ya kupambana na rushwa katika mkutano wa Novemba mwaka huu.

Nchi hiyo iliweka sharti la kutoa msaada kutunisha bajeti kuu ya serikali na asilimia 20 ya fedha zilizoahidiwa zilihusishwa na kurekebisha sheria ya kupambana na rushwa kwa sharti kwamba muswada huo upelekwe bungeni Novemba 2006.

Taarifa iliyotolewa na Ubalozi wa Denmark nchini imesema kuwa kuwasilishwa kwa sheria mpya ya kupambana na rushwa bungeni ilikuwa ni mojawapo ya kipimo cha utekelezaji, kilichokubaliwa na serikali ya Tanzania na washirika wa maendeleo wanaoichangia bajeti ya serikali mwanzoni mwa mwaka huu.

Taarifa hiyo iliyotiwa saini na Katibu wa Kwanza wa Ubalozi huo, Jacob Dal Winther, imeeleza kuwa sheria mpya ya kupambana na rushwa inatarajiwa kuwa ni nyenzo muhimu katika kuimarisha vita dhidi ya rushwa.

Alisema sheria hiyo inaweka mazingira ya kupata taarifa na inatoa uwezekano wa kuwaadhibu watu wanaothibitika kuwa ni wala rushwa na pia inalinda watu wanaotoa taarifa za vitendo vya rushwa.

"Kutokana na umuhimu wa sheria hii kwa Tanzania, Denmark ilikubaliana na serikali ya Tanzania kuwa asilimia 20 ya fedha za msaada itakazotoa kwa ajili ya bajeti ziunganishwe na kipimo hiki maalum. Hata hivyo sheria hii haikuweza kuwasilishwa bungeni mwezi Novemba kama ilivyokubaliwa," inasema sehemu ya taarifa hiyo.

Wakati huo huo, Denmark imekubali kuipatia Tanzania msaada wa bajeti wa Sh109 bilioni wa kipindi cha miaka 2006-2010. Sambamba na msaada huo, Denmark inatoa kiasi cha Sh22 bilioni kusaidia kuboresha sekta ya umma katika maeneo ya utumishi wa umma, usimamizi wa fedha za umma na maboresho ya sekta ya sheria.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.