Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mtandao wa ujambazi wasambaratishwa
Mtandao wa ujambazi wasambaratishwa
By Habari Tanzania | Published  12/12/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mwandishi Wetu

POLISI mkoani Morogoro wamedai kuusambaratisha kabisa utandao wa ujambazi baada ya kumkata mtuhumiwa wa mwisho ambaye walikuwa wakimsaka kwa udi na uvumba.

Mtuhuhumiwa huyo ambaye ni mkazi wa mkazi wa Mjipya katika Manispaa ya Morogoro, alikamatwa Ijumaa iliyopita alfajiri wakati ameweka mitego yake ya kuwanasa wapita njia kwenye kilabu cha pombe za kienyeji cha Kaloreni kilichopo jirani na makazi yake.


"Mtuhumiwa huyu amekuwa akisakwa kwa muda mrefu sasa kutokana na matukio mbalimbali ya uporaji wa kutumia silaha... alikuwa amebaki peke yake baada ya kuvunjwa kwa mtandao wao, akiwepo kaka yake ambaye alishakamatwa na kesi yake ipo mahakamani," alisema jana Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Morogoro, Hemedi Msangi wakati akizungumza na waaandishi wa habari ofisini kwake.

Baada ya kukamatwa, inadaiwa kuwa, mtuhumiwa huyo aliwaelekeza polisi maeneo ambako alikuwa akiuza vitu mbalimbali alivyokuwa akipora na kukamata baiskeli 11.

Mtuhumiwa huyo inadaiwa kuwa anamiliki bunduki ambayo hadi sasa bado haijapatikana na polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi ili kubaini mahali ilipo.

Wakati huo huo; watu nane wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukamatwa na nyaya za umeme mali ya Shirika la Umeme nchini (TANESCO) Mkoa wa Morogoro

Watu hao walikamatwa Desemba 8, majira ya alfajiri katika maeneo ya Mafisa na barabara ya Uhuru mjini hapa, wakiwa na nyaya hizo nyumbani kwao.

Miongoni mwa watu hao, ndugu wawili ambao ni wanunuzi wa nyaya hizo, wakazi wa Mtaa wa Uhuru na wengine ni walioiba, wakazi wa Mafisa.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.