Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Polisi jela kwa kuua raia kwa risasi
Polisi jela kwa kuua raia kwa risasi
By Habari Tanzania | Published  12/6/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Paulina David

MAHAKAMA€ Kuu Kanda ya Mwanza, imemuhukumu aliyekuwa askari la Jeshi la Polisi, E 7869 PC Ezra Kaira (35) kutumikia kifungo cha miaka 10 jela kwa kosa la kumuua Mlima Mashaka kwa kumpiga risasi kichwani.

Hukumu hiyo ilitolewa juzi mahakamani hapo na Hakimu Mkazi Mfawidhi mwenye mamlaka ya kusikiliza kesi za Mahakama Kuu Federika Mgaya.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Mgaya alisema kuwa, €mahakama hiyo imetoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwa mshtakiwa huyo na watu wengine wenye tabia ya kuua raia bila kosa.

Awali kabla ya kutoa hukumu hiyo, Hakimu Mgaya alitoa nafasi kwa mshitakiwa huyo kutoa shufaa zake ili apunguziwe adhabu.

Akijetetea mahakamani hapo, mshtakiwa huyo aliiomba impunguzie adhabu kwa kuwa mke, mtoto na wazazi wake wanamtegemea.

Awali Wakili wa Serikali, Edwin Kakolaki aliimbia mahakama kuwa, Julai 13 mwaka 2001 usiku katika eneo la Nera na Barewa jijini Mwanza, askari huyo akiwa na wenzake wawili kwenye doria, walikutana na dereva teksi aliyewaambia amewaona watu kama majambazi eneo la Mlima wa Machemba.

Alisema askari huyo na wenzake walianza kuwafuatilia hadi walikoelekezwa, baada ya kuwaona walikimbia.

Mwendesha mashtaka huyo alisema kuwa, mshtakiwa na wenzake, waliendelea kuwafuatilia€watu hao hadi eneo la Mkanyeye, lakini walikimbia na kujificha kwenye jumba moja.

" Mara baada ya mshtakiwa na wenzake kufika huko, walikutana na mlinzi ambaye aliulizwa kuwa amewaona watu waliokimbia, aliwaonyesha na kufanikiwa kumkamata Mlima Mshaka na kumwamuru kulala chini," alisema na kuongeza kuwa:

" Mshtakiwa aliwaagiza wenzake watafute kamba ili wamfunge na kumpeleka kituoni, wakati wenzake wakitafuta kamba, walisikia mlio wa risasi na walipokwenda eneo la tukio walikuta Mlima ameuawa kwa kupigwa risasi ya kichwani."


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.