Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  19 wabainika kughushi vyeti Wizara ya Maji
19 wabainika kughushi vyeti Wizara ya Maji
By Habari Tanzania | Published  12/5/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:
Na Mwandishi Wetu
 
WATUMISHI 19 katika Wizara ya Maji wamebainika kwamba walijipatia ajira kwa kutumia vyeti vya kughushi.
 
Taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Patrick Rutabanzibwa imesema Wizara imehakiki vyeti vya watumishi wake walioajiriwa Mei na Agosti, mwaka huu na kubaini kuwa 19 kati ya 63 walioajiriwa walitumia vyeti vya kughushi ili kupata ajira.
 
Taarifa ya Katibu Mkuu ilisema kazi ya kuhakikisha vyeti ilifanyika kati ya Oktoba na Novemba, mwaka huu kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Maji na Baraza la Mitihani la Taifa.
 
Kwa mujibu wa taarifa vyeti vilivyobainika kuwa ni vya kughushi ni vya kidato cha nne na walioabainika kuwa na vyeti hivyo ni Mafundi Sanifu wawili, Karani wa Masjala mmoja, katika Muhtasi mmoja na madereva 15.
 
Rutabanzibwa alisema suala hilo limeripotiwa polisi kwa hatua za kisheria na tayari baadhi ya watuhumiwa wamesimamishwa kazi na wanahojiwa na Jeshi la Polisi.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.