Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Watu 10 wakamatwa kwa dawa za kulevya
Watu 10 wakamatwa kwa dawa za kulevya
By Habari Tanzania | Published  12/2/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Mwandishi Wetu

JESHI la polisi likishirikiana na polisi wa kimataifa (Interpol) limewakamata wafanyabiashara maarufu 10 wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya.

Akizungumza jijini Dar es salaam jana, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya jinai Robert Manumba, alisema watu watano kati ya 10 waliokamatwa wamekwisha kufikishwa mahakamani.

Manumba alisema dawa hizo ambazo ni heroin na cocaine zinatoka katika nchi za India, Pakistan, Iran na Norway

Alisema operesheni ya kuwakamata wafanyabiashara wa dawa hizo, wakiwa ni pamoja na watumiaji na mawakala, inafanyika kwa ushirikiano wa polisi wa kimataifa (Interpol) na Jeshi la Polisi.

Manumba alisema kila kona nchi kuna mitego ambayo wameshaiweka kwa ushirikiano huo ili kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wanaojihusisha na biashara hiyo wanatiwa nguvuni.

Akizungumzia bangi, alisema mikoa ya Arusha, Iringa na Mbeya imegundulika kuwa na mashamba mengi ya bangi ambayo baadhi wameweza kuyateketeza na bado wanaendelea kuyasaka mengine.

Alisema makosa ya kijinsia pia yameongezeka kwa kiasi kikubwa ambayo ni pamoja na ubakaji na ulawiti hasa watoto wadogo.

Akitoa tathimini ya hali ya uhalifu nchini, Manumba alisema kwa upande wa ujambazi, uhalifu huo umepungua lakini jeshi la polisi linaelekeza macho yake kwa na nguvu zake zote katika benki za wananchi Saccos.

Alisema lengo ni kuiweka nchi katika hali ya amani na usalama na kwamba jeshi hilo limedhamiria kuweka ulinzi wa uhakika katika benki hizo zilizopo sehemu mbalimbali nchini.

Kuhusu ajali barabarani alisema kuwa bado ni tatizo, kutokana na uzembe wa madereva, ambao wanakuwa hawajali maisha ya watu wengine.

Alisema kutokana na ongezeko la ajali Jeshi la Polisi limeunda kamati kwa kushirikiana na wamiliki wa magari, madereva, Tanroads, watumiaji wa barabara na sumtara.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.