Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Rais ateua mrithi wa Ditopile
Rais ateua mrithi wa Ditopile
By Habari Tanzania | Published  12/2/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Mwandishi Wetu

RAIS Jakaya Kikwete amemtaeua Abeid Mwinyimusa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora kuanzia Novemba 28, mwaka huu.

Uteuzi huo uliotangazwa na katika taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, unaziba nafasi ya Ditopile Mzuzuri aliyejiuzulu hivi karibuni kutokana tuhuma za mauaji ya dereva wa daladala zinazomkabili.

Kabla ya kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa huo, mwinyimusa alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mjini. Mwinyimusa ataapishwa na Rais Kikwete Jumatatu Desemba 4, mwaka huu.

Vile vile, siku hiyo, Kikwete atawaapisha Balozi Patrick Mombo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Edward Hosea kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya kuzuia Rushwa (Takuru).


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.