Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Denti Dar amtwisha magumi Polisi
Denti Dar amtwisha magumi Polisi
By Habari Tanzania | Published  06/6/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Askari polisi mwenye namba 3399 PC George amepewa mkong’oto wa nguvu ambao kama si kudra za Mwenyezi Mungu huenda ungemuacha kibogoyo.

Askari huyo anadaiwa kupewa kibondo hicho na mwanafunzi Deogratius Paul, 17, anayesoma Ubungo Maziwa Jijini.

Hata hivyo denti huyo anayedaiwa kujifanya Tyson, ameburuzwa katika Mahakama ya Mwanzo Manzese.

Hati ya mashitaka iliyosomwa na karani wa mahakama hiyo, Janeth Mwanisawa imedai mbele ya hakimu, Slyvester Nyanda kuwa, mshtakiwa alitenda kosa hilo Mei 24 mwaka huu, saa 2:00 usiku huko Ubungo.

Mahakama ikaambiwa siku hiyo kuwa, mshtakiwa kwa makusudi na huku akijua kufanya hivyo ni kosa alimpora mlalamikaji mwenye namba 3399 PC George pesa taslimu Sh. 105,000 baada ya kumpiga ngumi tatu mdomoni, tendo ambalo ni kinyume cha kifungu cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu namba 269 sura ya 16.

Mshtakiwa amekana shtaka hilo na yuko nje kwa dhamana hadi Juni 6 mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Wakati huohuo, Mlemba Hatibu mlinzi wa Shirika la Umeme Nchini, Tanesco amemfikisha kizimbani Wilbard Mwaipopo, 26, mkazi wa Ubungo Jijini, akimshitaki kwa wizi.

Mshtakiwa anadaiwa kutenda kosa hilo Mei 16 mwaka huu, saa 8:00 usiku huko Ubungo.

Ikadaiwa siku hiyo kuwa, mshtakiwa aliiba nati na vifaa vingine vya umeme vyenye thamani ya Sh. 150,000 tendo ambalo ni kinyume cha kifungu cha sheria namba 265 sura ya 16.

Mshtakiwa amekana shtaka hilo na yuko rumande kwa kukosa wadhamini hadi Juni 6 mwaka huu, kesi hiyo itakapotajwa tena.

Katika kesi nyingine, Hamis Khassim, 20, mbeba mizigo na mkazi wa Manzese Jijini, amekana shtaka la kufanya fujo.

Mshtakiwa anadaiwa kutenda kosa hilo Mei 22 mwaka huu, saa 1:00 jioni huko Manzese Tip Top.

Ikadaiwa siku hiyo kuwa, mshtakiwa alimfanyia fujo mlalamikaji, Halidi Said kwa kumwaga chipsi, mayai na kuharibu kabati vyote vikiwa na thamani ya Sh. 37,000 mali ya mlalamikaji huyo, tendo ambalo ni kosa kisheria.

Mshtakiwa amekana shtaka hilo na yuko rumande kwa kukosa wadhamini hadi Juni 6 mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.