Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Ramadhan Semtawa  »  Taasisi ya moyo kuanza kutibu figo
Taasisi ya moyo kuanza kutibu figo
By Ramadhan Semtawa | Published  11/27/2006 | Ramadhan Semtawa | Unrated

Na Ramadhan Semtawa

TAASISI ya moyo nchini (THI) inatarajia kuimarisha Idara yake ya Figo kama hatua ya kuboresha huduma zake za matibabu ya moyo.

Hatua hiyo inatokana na matatizo ya moyo hasa upasuaji kuwa na mahusiano na matatizo ya figo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki wakati wa kuutambulisha ujumbe wa wataalamu watano wa magonjwa ya moyo ikiwemo upasuaji, kutoka Ujerumani ambao umekuwepo nchini, mwanzilishi wa THI, Ferdinand Massawe, alisema mara nyingi wagonjwa wanaohitaji kufanyiwa upasuajai hukutwa pia na haja ya kusafishwa figo.

Massawe alisema kutokana na kubaini kuwepo mahusiano hayo ndiyo maana taasisi hiyo imeamua kuimarisha idara hiyo.

"Tumeanza mikakati ya kuimarisha idara yetu ya figo, tumebaini wakati mwingine wagonjwa wetu wa moyo wanahitaji kusafishwa figo," alifafanua Dk Massawe.

Dk Massawe alisema kwa sasa THI imejipanga vema na kwamba kama ni uwezo inaweza kufanya upasuaji kwa watu wawili kwa siku.

Alisema kwa sasa inasubiri kutia saini mkataba na serikali utakaoipa jukumu la kufanyia upasuaji wagonjwa wa matatizo ya moyo badala ya kuwapeleka nje.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.