Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mbwa waua fundi umeme
Mbwa waua fundi umeme
By Habari Tanzania | Published  11/27/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Mussa Juma

FUNDI umeme, mkazi wa eneo Mianzini mjini hapa, Abraham Maenda(33) amefariki baada ya kushambuliwa na kundi kubwa la mbwa ambao wamekuwa wakijikusanya katika eneo la Mianzini nyakati za usiku.

Kamanda wa polisi mkoani hapa, Matei Basilio akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema kundi hilo la mbwa ambao wamekuwa wakilalamikiwa kwa muda mrefu lilimvamia fundi huyo wakati akirejea nyumbanikwake.

Kamanda Basilio alisema Maeda aliumwa na mbwa hao hadi kufariki baada ya kumzidi nguvu.

Hata hivyo, alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa Maeda aliweza kuvamiwa na mbwa hao na kujeruhiwa sana kwa kuwa alikuwa amelewa, hivyo alishindwa kupambana nao.

Kamanda Basilio alisema kutokana na tukio hilo, anawasiliana na maafisa kadhaa wa mkoa wa Arusha ili kuhakikisha kuwa wanaanza msako mkali wa kuwaua mbwa hao.

“Ni kweli eneo la Mianzini limekuwa na mbwa wengi ambao wanatembea ovyo, hivyo tunawasiliana na wahusika ili kuanza kuwaua mbwa hao,” alisema Basilio.

Katika tukio jingine, Mtoto, Hamis Yusuph(1) amefariki juzi katika eneo la Mianzini baada ya kutumbukia kwenye shimo la shoo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.