Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Tanzania yasema haiwezi kumezwa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Tanzania yasema haiwezi kumezwa Jumuiya ya Afrika Mashariki
By Habari Tanzania | Published  11/26/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri wa Ushirikiano Afrika Mashariki, Dk Diodorus Kamala, amesema wanaofikiri kuwa Tanzania ikiingia kwenye Shirikisho la Afrika Masharika, itakuwa 'shamba la bibi' la kuvuna kila mtu wanajidanganya.

"Litakuwa shirikisho ambalo halitafanya Tanzania kuwa kichwa cha mwendawazi, ambacho kila mtu hujifunzia kunyoa. Tanzania haitakuwa shamba la bibi ambalo kila mtu kuja kuvuna anavyotaka. Itabaki Tanzania kwa maslahi ya Watanzania," alisema.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na jumuiya ya Chuo Kikuu Mzumbe na Chuo Kikuu cha Waislam Morogoro, Dk Kamala alisema Rais Jakaya Kikwete ameamua maoni yatakayotolewa na wananchi jinsi ya kujiunga kwenye shirikisho ndio yataheshimiwa.

Alivitaka vyombo vinavyosimamia sheria kufanya kazi zake kwa mujibu wa sheria.

Kauli hiyo ilifuatia maoni ya baadhi ya wasomi kuonyesha wasiwasi jinsi Ziwa Victoria lilivyovamiwa na wavuvi kutoka Kenya na Uganda, huku wavuvi wa Tanzania wakiwa hawaruhusiwi kuvua sehemu za nchi hizo.

"Nani kawambia kuwa mipaka ya Ziwa Victoria imeondolewa? Mipaka ipo na haitaondolewa ingawa baadhi ya wanachama wa EAC wanataka tufanye hivyo, lakini hatuwezi kwa sababu Tanzania itabaki kwa maslahi ya Watanzania, kinachotakiwa ni vyombo vyetu vya kusimamia sheria kufanya kazi zake kikamilifu," alisema Dk Kamala.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by Dua)
    Rating
    Unapokuwa na rais mmoja wa jumuiya ya afrika mashriki maana yake ni nini?

    Mbona Dk. Kamala huweki hiyo mikataba watu tuione?
    Ni mambo ya uzandiki kutupigia porojo bila kutuwekea mikataba bayana tuione. Hivi sasa wewe binafsi kama jumuiya haipo huna mshahara ndio sababu inapigia debe.

    Wekeni wazi mamlaka ya huyo rais na majukumu yake acheni ubabaishaji, bado hatujalala haya ndio mambo yanayoleta fujo kule Zanzibar mpaka leo na hamjaweza kutatua suala hilo - mnaanza kutuletea muungano mwingine, acheni uongo

     
Submit Comment


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.