Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Barrick walalamikia wanaowakwamisha
Barrick walalamikia wanaowakwamisha
By Habari Tanzania | Published  11/23/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mwandishi Wetu, Tarime

KAMPUNI ya Barrick Tanzania inayomiliki mgodi wa dhahabu wa North Mara, imesema inakwazwa kupanua uwekezaji wake nchini kutokana na watu wachache kwa masilahi binafsi.

Meneja Mkuu wa mgodi huo, Bill MacNevin, aliwaambia waandishi wa habari waliotembelea mgodi huo uliopo eneo la Nyamongo mkoani Mara kuwa kampuni yake inapenda kuona wadau wote wakishirikiana.

“Tunakatishwa tamaa kwa karibu kila kitu cha maendeleo tunachofanya, watu wachache tu wanawachochea baadhi ya wanavijiji ili wasishirikiane nasi,” alisema.

Kauli ya MacNevin ilitokana na taarifa zinazodaiwa kuenezwa na shirika lisilo la kiserikali kuwa mgodi huo umekuwa ukiwalazimisha wanavijiji kuhama ili kupisha uchimbaji wa madini.

Alisema kuwa mgodi wake una mipango mikubwa ya uwekezaji katika eneo hilo, na kuongeza kuwa hilo linaweza kufanyika kama wadau wote watashirikiana na kampuni yake.

“Tuna mipango ya kujenga bwawa kubwa kwa ajili ya kutunza maji machafu kutoka mgodini, lakini watu wawili wamekataa kuhama kutoka kwenye ardhi yao bila sababu yoyote ya msingi pamoja na kutoa fidia kubwa,” alisema bila kutaja kiasi hicho.

Alisema kuwa kampuni yake ina sera ya kuwajengea nyumba za kisasa wanavijiji wanaohama maeneo yao kwa hiari na pia kuwapa fedha nyingi kama fidia.

“Kwa sasa kuna watu wawili tu katika eneo hili wanaomiliki ekari nne tu ambao wamegoma kuhama pamoja na serikali kuwataka wafanye hivyo,” alisema.

Alisema kuwa juhudi za pamoja zinahitajika katika ngazi za wilaya na mkoa kuhakikisha kuwa wawekezaji wanapata mazingira mazuri ya kufanya kazi.

Alisema kuwa mgodi wake umekabidhi sh milioni 100 kwa wanasheria kama dhamana ili wanavijiji wanaohamishwa waweze kulipwa, lakini wanavijiji hao wamegoma.

Barrick Tanzania imewekeza sh zaidi ya trilioni moja. Imeajiri Watanzania 4,511


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.