Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Idadi ya watalii Tanzania yaongezeka
Idadi ya watalii Tanzania yaongezeka
By Habari Tanzania | Published  11/17/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Mwandishi Wetu

IDADI ya watalii wa kigeni wanaoingia nchini imeongezeka kutoka 582,807 mwaka 2004 hadi 612,754 mwaka jana.

Ongezeko hilo limeongeza mapato kutoka dola za Marekani 746.02 milioni mwaka 2004 hadi dola 823.59 mwaka jana ambazo ni sawa na ongezeko la asilimia 10.12.

Matarajio ya mwaka 2006/07 ni kupata watalii wa kigeni 700,000 ambao wataliingizia taifa dola 900 milioni.

Hata hivyo, kwa mujibu wa ripoti ya utalii ya mwaka 2005, juhudi za kutangaza vivutio vya utalii Tanzania bado ni ndogo ukilinganisha na sehemu nyingi duniani na kuwa fedha zinazotengwa na serikali kwa ajili ya kazi hiyo ni ndogo.

Ripoti hiyo imelinganisha juhudi za kutangaza utalii baina ya nchi na nchi, na kubaini kuwa katika bajeti ya mwaka jana, wakati Bodi ya Utalii Tanzania ilitengewa dola 1.5 milioni, Bodi ya Utalii ya Kenya ilipewa dola 15 milioni, Afrika Kusini dola 150 milioni wakati Malaysia ilitengewa dola 100 milioni.

Ripoti hiyo imebainisha zaidi kwamba, watalii wengi ambao huingia nchini hutumia usafiri wa njia ya anga na kwamba mwaka jana walikuwa ni 330,587 ikilinganishwa 257,195 waliotumia usafiri huo mwaka 2004.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.