Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wauza nyama kortini kwa kuwapunja wateja
Wauza nyama kortini kwa kuwapunja wateja
By Habari Tanzania | Published  11/17/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Mwandishi Wetu

WAFANYABIASHARA wawili wa duka la nyama, David Maungo (29) na Edward Galagaja (22) wakazi wa Tegeta, Kinondoni juzi wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakidaiwa kuwauzia wateja nyama yenye uzito pungufu.

Mwendesha Mashtaka kutoka Wakala wa Vipimo, Moses Mbunda, alidai mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Said Msuya kwamba washitakiwa walitenda kosa hilo Novemba 12, mwaka huu huko Tegeta, jijini.

Mbunda alidai Mahakamani hapo kwamba Maungo na Galagaja walikutwa wakimuuzia nyama Maango Kitwana Rajabu kwa kutumia jiwe la kilo mbili lenye upungufu wa uzito wa gramu 450.

Mwendesha Mashtaka alidai zaidi kuwa kwa kuuza nyama ambayo haikufikia uzito unaotakiwa, walitenda kosa kinyume cha vifungu Na 35 (i), 51 (i) na 45 (i) vya Sheria Na 20 ya Vipimo ya mwaka 1982.

Washtakiwa wote wawili walikana mashtaka dhidi yao na wamerudishwa rumande baada ya kukosa wadhamini hadi Novemba 29, kesi hiyo itakapotajwa tena. Upelelezi wa kesi hiyo unaendelea.

Kwa mujibu wa kifungu Na 45 cha Sheria hiyo, washtakiwa wanaweza kutozwa faini ya Sh10,000 au kifungo cha miaka mitatu jela ikiwa itathibitishwa na mahakama kwamba wametenda kosa hilo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.