Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mkuu wa mkoa akerwa na maderva wa daladala
Mkuu wa mkoa akerwa na maderva wa daladala
By Habari Tanzania | Published  11/16/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, William Lukuvi, amesema sekta ya usafiri wa nchi kavu na majini mkoani hapa imegubikwa na matatizo mengi yakiwemo ya watoa huduma ya mabasi ya daladala kutoa huduma isiyoridhisha, ikiwa ni pamoja na kutoa lugha chafu kwa abiria.

Lukuvi alisema hayo jana kwenye mkutano wa wadau wa sekta ya usafiri wa nchi kavu na majini, ulioandaliwa na Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini(Sumatra) na kufanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Alisema kitendo cha watoa huduma ya usafiri, hasa wa mabasi ya daladala kutoa lugha chafu kwa abiria, kuwabughudhi wanafunzi na kutoza nauli wanazotaka, kumesababisha wakazi wa mkoa huo kukata tamaa na usafiri huo.

Alisema hali hiyo imekuwa kukichangiwa na mambo mengi yakiwemo ya miundombinu dhaifu iliyopo katika mkoa huo na utendaji mbaya wa mamlaka na taasisi husika katika kusimamia na kudhibiti watoa huduma ya usafiri.

Alisema tatizo lingine ni elimu ndogo ya haki na wajibu wa watumiaji katika kuboresha huduma za usafiri kama uzembe wa wahudumu na waendesha vyombo vya usafiri, kama vile madereva na makondakta kutofuata sheria za usalama barabarani na ukiukwaji wa sheria za uendeshaji biashara ya usafiri wa abiria.

Alisema mkutano huo wa wadau wa huduma ya usafiri wa majini na nchi kavu kumekuja wakati muafaka ambapo mkoa umepania kupunguza matatizo yanayotokana na huduma ya usafiri isiyoridhisha.

Hata hivyo, alisema hivi sasa mkoa wa huo una mtandao wa barabara wenye jumla ya kilometa 5554.2.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.