Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Vileo marufuku makazi ya watu Zanzibar
Vileo marufuku makazi ya watu Zanzibar
By Habari Tanzania | Published  11/16/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Salma Said, Zanzibar

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imepiga marufuku utoaji wa leseni za vileo katika maeneo wanaoishi watu na nyumba za ibada.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Vikosi vya SMZ, Suleiman Othman Nyanga aliyasema hayo juzi wakati akizindua mahakama ya vileo ofisini kwake Vuga, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Mahakama ya vileo imeanzishwa maalum visiwani hapa ili kushughulikia na kusimamia vilabu vyote na uendeshaji wake.

Vile vile mahakama hiyo itakuwa inapokea malalamiko ya wananchi juu ya vilabu vilivyofunguliwa maeneo mbalimbali, kutoa maamuzi ya malalamiko hayo na kuangalia nidhamu za vilabu.

Nyanga alisema kumejitokeza malalamiko mengi kuhusu kuwepo kwa vilabu vya pombe karibu na makazi ya wananchi pamoja na nyumba za ibada jambo ambalo limekuwa likilalamikiwa na wananchi wengi.

“Tuwe waangalifu sana katika suala la utoaji wa leseni za vileo...yapo malalamiko mengi kwamba leseni zinatolewa bila ya kufanya utafiti wa kina,” alisema Nyanga.

Alisema utoaji ovyo wa leseni usiozingatia maadili umekuwa ukileta ufumbufu kwa wananchi katika maeneo yanayokaliwa na watu.

Alisema mara nyingi wananchi huwa wanavurumishiana maneno ya ovyo jambo ambalo huzusha malalamiko mengi na wakati mwengine ugomvi wa mara kwa mara kati ya wamiliki wa baa na jirani zao.

Alisema utoaji wa leseni za vileo katika makazi ya wananchi husababisha kuvuruga maadili ya vijana, utamaduni na kuchochea vitendo vya kihuni.

Mwenyekiti wa Mahakama ya Vileo, Abdulrazak Abdulkadir, alisema mahakama yake itakuwa makini katika utoaji wa leseni kwa wamiliki wa baa hizo.

Alisema jambo la kwanza watakaloangalia ni mazingira ya mahali panapotaka kufunguliwa baa, na kwamba endapo ni sehemu iliyo karibu na msikiti au kanisa, hawatatoa kibali.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.