Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Vigogo polisi waapishwa kuunda tume
Vigogo polisi waapishwa kuunda tume
By Habari Tanzania | Published  11/11/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:

Na Elizabeth Mjatta

MAAFISA watano wa polisi, akiwemo Inspekta Jenerali Saidi Mwema, jana wameapishwa katika Mahakama Kuu ya Tanzania kuwa wajumbe wa tume ya utumishi ya polisi na magereza.

Wengine walioapishwa ni pamoja na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DPP) Robert Manumba, Mkurugenzi wa Utawala, Levinus Mbuya, Kamishina wa Utawala na Fedha, Clodwig Mtweve na Shaban Mlubi.

Wajumbe hao waliapa mbele ya Jaji Thomas Mihayo, ambaye aliwataka kufanya kazi kwa bidii kwani kazi hiyo ni nyeti na muhimu katika kujenga jeshi imara na lenye heshima kwa jamii.

Alisema yeye binafsi ameridhishwa na uamuzi wa jeshi hilo kutoa namba za simu za maafisa wa ngazi za juu kwa umma ikiwa njia mojawapo ya kupambana na uhalifu hapa nchini.

“Sio mimi tu, hata wananchi wengi wamekuwa na imani kwa jeshi lao kutokana na viongozi kuwa wawazi kwa umma hivyo hali hii inailirudishia jeshi hilo heshima,” alisema Jaji Mihayo.

Wajumbe hao walioapishwa watakuwa na kazi mbalimbali katika tume hiyo, ikiwamo kushughulikia masuala ya nidhamu katika jeshi, kuwapandisha vyeo askari wanaofanya vizuri katika jeshi hilo na kushughulikia masuala ya adhabu na makosa mabalimbali


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by McFallan)
    Rating
    Hii ni tume ya utumishi ya Polisi na Magereza au ya Polisi? Mbona hakuna mtu wa magereza? Haitakuwa "biased"?
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.