Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Ramadhan Semtawa  »  Ushindani waitisha TPDC
Ushindani waitisha TPDC
By Ramadhan Semtawa | Published  11/11/2006 | Ramadhan Semtawa | Unrated

Na Ramadhan Semtawa

USHINDANI wa kibiashara katika soko la mafuta umelitisha Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini (TPDC) na sasa limedai linafanya mambo yake chini kwa chini kwa kuogopa washindani.

Hatua hiyo inatokana na TPDC kuwasilisha ripoti yake ya kibiashara Wizara ya Nishati na Madini, huku ikikataa kuitoa hadharani.

Taarifa kutoka ndani ya Wizara ya Nishati na Madini na TDPC, zinasema katika ripoti hiyo, TPDC imetoa mwelekeo wa kibiashara kuanzia ununuzi, miundombinu na wadau itakaoshirikiana nao katika kuingiza mafuta.

"Tayari TPDC imekwisha kuwasilisha ripoti yake, ina mambo mengi, kikubwa inatoa mwelekeo wa kibiashara kuanzia ununuzi wa mafuta hadi kuyaingiza nchini," kilisema chanzo hicho kutoka wizarani.

Akizungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana kuhusu ripoti hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, Yona Killagane, alisema hadi sasa mipango yote ya utekelezaji wa agizo la serikali kuhusu uagizaji mafuta inakwenda vizuri.

Hata hivyo, Killagane alisema kutokana na ushindani mkubwa wa kibiashara, shirika lake haliwezi kuanika hadharani mipango yake ya kibiashara.

Killagane alisema TPDC itafanya biashara katika mfumo wa ushindani tofauti na miaka ya nyuma wakati dola ilipokuwa ikihodhi uchumi, hivyo ni lazima ichukue tahadhari kutoka kwa washindani wake.

"Hadi sasa utekelezaji agizo la serikali unakwenda vizuri, ripoti zetu za kibiashara hatuwezi kuziweka hadharani kwa sababu washindani wetu wanaweza kuzitumia na kutukwamisha katika baadhi ya mambo," alisisitiza Killagane.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Is Tanzania a safe place to invest?
  4. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Linda Garner
  4. Nthelezi Nesaa
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.