Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Kampuni sita zataka kuchimba makaa ya Mchuchuma
Kampuni sita zataka kuchimba makaa ya Mchuchuma
By Habari Tanzania | Published  11/10/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
MAKAMPUNI sita kutoka nchi za Kenya, Uganda, Afrika Kusini, Australia, India na Israel, yameonyesha nia ya kuwekeza kwenye mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma.
 
Hata hivyo pamoja na makampuni hayo kujitokeza bado serikali haijaamua kuutoa mradi huo kwa mwekezaji, ikitafuta kwanza tafsiri sahihi ya kumpata mwekezaji ambaye atazingatia maslahi ya taifa na ya kwake.
 
Hayo yalielezwa bungeni jana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Benard Membe, alipokuwa akijibu swali ya mbunge wa Masasi, Raynald Alfons, aliyetaka kujua mikakati ya serikali ya kuyatumia makaa ya mawe ili kuzalisha nguvu za umeme.

Alisema kuwa kutokana na umuhimu wa kulinda maslahi ya taifa, kama vile bei ya umeme endelevu, utunzaji wa mazingira na ukubwa wa mradi huo ambao unaunganishwa na uendelezaji waa mradi wa chuma wa Liganga, serikali inabidi iwe makini katika kupata mwekezaji atakayezingatia masuala hayo muhimu kwa taifa.
 
Hata hivyo, Membe, alisema serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC), iliunda kamati ya wataalamu ili kupitia mapendekezo na kupendekeza njia nzuri za kumpata mwekezaji ambaye atazingatia maslahi ya pande zote mbili.

Alisema mradi huo wa Mchuchuma umeingizwa katika mpango wa maendeleo wa Mtwara Corridor ambao upo chini ya Wizara ya Miundombinu na mpango wa Power Sector Master Plan (PSMP) wa miaka 25 Aliongeza kwamba mradi huo unaainisha vyanzo muhimu ikiwemo nishati mbadala ya uzalishaji umeme kwa kutumia makaa ya mawe, ukubwa wa mradi, makisio ya gaharama na wakati muafaka wa kutekeleza mradi. .

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.