Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Tanzania,Msumbiji kuondoa viza
Tanzania,Msumbiji kuondoa viza
By Habari Tanzania | Published  11/8/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

BUNGE limepitisha mkataba wa kuondoa viza kati ya Tanzania na Msumbiji na kinachosubiriwa sasa ni ridhaa ya Rais ili utekelezaji wake uanze.

Lengo la kuu la mkataba huo ni kuondoa matumizi ya viza kwa hati za kusafiria za kidiplomasia, utumishi wa umma na za kawaida kwa wananchi wa nchi hizo mbili na kuanzia sasa watakuwa wanatembeleana bila ya kikwazo hicho.

Nchi hizo mbili ziliingia mkataba huo wa kuondoa matumizi ya viza Oktoba 10, mwaka jana na ulikuwa unasubiri kuridhiwa na Bunge.

Akisoma mkataba huo bungeni jana, Waziri wa Mambo ya Ndani, Joseph Mungai, alisema hatua hiyo itazidi kuimarisha husiano baina ya Tanzania na Msumbiji.

Alisema ibara ya tisa ya mkataba huo, inahitaji kukamilika kwa taratibu za kisheria ili makubaaliano yaliyoainishwa kwenye mkataba yaweze kutumika.

Akisoma maoni ya Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama kuhusiana na mkataba huo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, William Kusila, alitahadharisha kuwa wakati wa utekelezaji wake, vyombo vya ulinzi na usalama viwe makini ili kukabiliana na changamoto zitakazojitokeza.

Alisema kuna uwezekano wananchi wasio waaminifu wa pande zote mbili wakatumia fursa hiyo kuendesha uhalifu kama biashara ya dawa za kulevya, uingizaji wa silaha kinyume cha sheria na ujambazi.

Kamati hiyo imependekeza vituo vya uhamiaji katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji ambao ni mrefu viongezwe na Watanzania wahamasishwe kutumia fursa za kiuchumi zitakazojitokeza.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.