Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Tanapa kununua ndege tatu
Tanapa kununua ndege tatu
By Habari Tanzania | Published  11/7/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
SHIRIKA la Hifadhi ya Taifa (Tanapa), lina mpango wa kununua ndege tatu kwa ajili ya kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji kwenye hifadhi.

Kati ya ndege hizo tatu, moja yenye uwezo wa kuchukua abiria 14 itafanya safari zake ikiwa ni pamoja na kutoa huduma ya usafiri kwa watalii watakaohitaji kwenda kutembelea hifadhi za kusini za Mahale iliyopo Kigoma, Katavi iliyopo Mpanda na Ruaha mkoani Iringa.

Hayo yalielezwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Zubein Mhita, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kahama, James Lembeli, aliyetaka kufahamishwa mipango ya serikali wa kupanua wigo wa utalii kwa kuzingatia bajeti ya mwaka huu wa fedha.

Mhita pia alisema kuwa wamiliki makampuni ya uwindaji wa kitalii wameruhusiwa kuendesha biashara ya utalii wa picha kwa miezi ambayo uwindaji wa kitalii haufanyiki.

Alisema hatua hiyo ina lenga kutanua wigo wa utalii hasa kwa kutoa fursa za kuendeleza utalii wa picha kwa maeneo yale yasiyokuwa na hifadhi za taifa.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.