Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mkuu wa mkoa Ditopile ashtakiwa kwa mauaji
Mkuu wa mkoa Ditopile ashtakiwa kwa mauaji
By Habari Tanzania | Published  11/7/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated

Na Tausi Ally

MKUU wa Mkoa wa Tabora, Kapteni Ukiwaona Ditopile Mzuzuri (58), amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa shtaka la mauaji ya dereva wa daladala, Hassan Mbonde.

Pamoja na mamia ya watu kufurika mahakamani, eneo la mahakama lilijaa ukimya wakati mkuu huyo wa mkoa akipandishwa kizimbani.

Ditopile anayekabiliwa na shtaka la mauaji kwa kutumia bastola, alifikishwa mahakamani hapo majira ya saa 3.09 asubuhi, akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi waliojaa kwenye magari mawili ya polisi aina ya Land Rover Defender.

Saa 3:54 asubuhi, Ditopile aliingizwa mahakama ya wazi, huku akiwa amevalia suruali yenye rangi ya kaki na shati la rangi mchanganyiko, miwani na mkononi wake wa kushoto ukiwa umefungwa bandeji.

Baada ya dakika mbili, Hakimu Michael Luguru, aliingia mahakamani na Mwendesha Mashtaka, Mrakibu wa Polisi, Germanusi Muhume, alimsomea Kapteni Ditopile shtaka la mauaji linalomkabili. Wengine waliokuwepo ni Mrakibu wa Polisi Naima Mwanga na Inspekta Raphael Rutaihwa.

Muhume alidai kuwa, Novemba 4, 2006 majira ya saa 1:00 usiku katika eneo la njia panda ya Bagamoyo na Kawe wilayani Kinondoni, Ditopile alimuua Hassan Mbonde.

Baada ya kusoma mashtaka, Muhume alisema kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na akaiomba mahakama ipange siku nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo.

Mtuhumiwa hakutakiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina uwezo wa kisheria kusikiliza shtaka linalomkabili. Mahakama Kuu ndio yenye uwezo wa kusikiliza mashtaka ya mauaji.

Kabla Hakimu Luguru, hajaaihirisha kesi hiyo hadi Novemba 20, mwaka huu, mawakili wanaomtetea mtuhumiwa, Dk Ringo Tenga, Losan Mbwambo, Cuthbert Tenga na Samwel Mapande, walidai kuwa siku ya tukio, mtuhumiwa aliumizwa mkono, hali iliyosababisha polisi kumpeleka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kufanyiwa matibabu.

Mawakili hapo hao waliiomba mahakama imruhusu mteja wao aonane tena na daktari wake ili kumpima afya yake.

Dk Ringo, aliomba mahakama imruhusu mtuhumiwa huyo afikishwe hospitali kwa kuwa anasumbuliwa na shinikizo la damu na pamoja na kisukari na kwamba, juzi shinikizo lilipanda hadi kufikia 180.

Wakili huyo alidai kuwa mteja wake pia ameshtushwa na gazeti moja lililoripoti kuwa, 'Ditopile Kunyongwa' akidai kwamba limemhukumu na kuongeza kuwa linaweza kumpeleka pabaya mtuhumiwa, hoja ambayo iliungwa mkono na upande wa mashtaka.

Baada ya Hakimu Luguru kuahirisha kesi hiyo majira ya saa 4:07, Ditopile aliingizwa kwenye gari ndogo ya saluni yenye vioo vya giza na kuondoka eneo la mahakama.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by washawasha)
    Rating
    Tunaomba mahakama na sheria ichukue mkondo wake katika kesi hiyo,na indapo mshtakiwa atakutwa na hatia na ni lazima awe nayo,afungwe kama wengine bila kujali cheo na madaraka aliyo nayo
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.