Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Ramadhan Semtawa  »  Viongozi Afrika wanastahili lawama
Viongozi Afrika wanastahili lawama
By Ramadhan Semtawa | Published  11/5/2006 | Ramadhan Semtawa | Unrated

Na Ramadhan Semtawa

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya chama cha NCCR-Mageuzi, Dk Sengodo Mvungi amewashutumu viongozi wa mataifa ya Afrika kwa uchu wao wa madaraka ambao umekuwa chanzo cha vita na machafuko yanayosababisha wakimbizi.

Alisema kutokana na uchu huo, viongozi wengi wa Afrika wamekuwa wakijaribu kuingia madarakani kwa kutumia njia za kuwagawa wananchi kidini, kikabila na hata kimajimbo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi wakati wa mkutano wa asasi zinazotoa msaada wa kisheria katika nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Dk Mvungi, alisema ni uongo kusingizia Wazungu kwamba wanaichafua Afrika.

Dk Mvungi aambaye alikuwa akizungumza katika mkutano huo uliaofanyika katika Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), jijini Dar es Salaam alieleza kwamba, hakuna ukoloni unaojipenyeza Afrika ambao unaweza kuwa chanzo cha machafuko isipokuwa viongozi wenyewe ndiyo chanzo.

"Uchu na uroho wa madaraka wa baadhi ya viongozi wetu wa Afrika ndiyo chanzo cha machafuko yanayozalisha wakimbizi barani Afrika," alisema Dk Mvungi na kuongeza,:

" Wanaingia madarakani kwa kutumia njia za kugawa wananchi kama udini, ukabila na hata ujimbo, matokeo yake wakiingia madarakani hutokea machafuko." alisi
sitiza.

Mwanataaluma huyo ambaye pia ni mwanasiasa, alisema hali hiyo pia iliikumba Tanzania, kule visiwani mwaka 2001 baada ya kuzalisha wakimbizi kwa mara ya kwanza ambao walikimbilia Shimoni, Mombasa.

Kwa upande mwakilishi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), tawi la Tanzania, Veronica Moday Ebi, alisema wakimbizi kama walivyo watu wengine wanapaswa haki zao za msingi za kibinadamu kama zilivyoanishwa katika Tamko la Dunia la Haki za Binadamu la mwaka 1948.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Is Tanzania a safe place to invest?
  4. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Linda Garner
  4. Nthelezi Nesaa
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.