ABIRIA 30 wamejeruhiwa baada ya mabehewa mawili ya treni ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) kuacha njia na kupinduka katika stesheni ya Kaliua, Mkoani Tabora.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Muhudi Mushihiri aliliambia Mwananchi Jumapili kwa simu kutoka Tabora kuwa katika ajali hiyo, watu 20 walitibiwa na kuruhusiwa kuendelea na safari yao kuelekea Mpanda, Mkoa wa Rukwa wakati wengine 10 walilazwa.
Alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo iliyotokea katikastesheni ya Kaliua hakijajulikana, lakini uchunguzi ulikuwa ukiendelea kwa kuhusisha maofisa wa polisi wa TRC.
Kamanda huyo alisema kuwa ajali hiyo ilitokea saa 3.40 asubuhi na kwamba hakuna mtu aliyepoteza maisha katika tukio hilo.