Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  TABOA yahimiza ushirikiano
TABOA yahimiza ushirikiano
By Habari Tanzania | Published  11/3/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mwandishi Wetu
 
MWENYEKITI wa Chama cha wenye Mabasi ya Mikoani nchini (TABOA), Mohamed Abdullah, amewataka wadau wa usafirishaji wa barabarani kutoa ushirikiano kwa mkakati uliotangazwa na Polisi katika kupunguza ajali za barabarani.
 
Abdullah alisema jana kuwa ni wakati mwafaka kwa watumiaji wa barabara kuwa na utamaduni wa kutumia barabara kwa kuzingatia misingi ya sheria zote za barabarani.
 
Pia alishauri wadau wa barabara wachukue utaratibu katika kuepukana na athari zinazoendana na ubovu wa barabara.
 
“Kwa kutumia nafasi yangu kama mwenyekiti wa TABOA, nitoe pongezi za dhati kwa serikali kwa kuunda chombo cha kudhibiti uendeshaji mbovu na wa kizembe barabarani,” alisema Abdullah, ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya mabasi ya Scandinavia Express.
 
Aliongeza kuwa TABOA inaahidi kutoa ushirikiano mkubwa kwa chombo hicho.
 
Mwishoni mwa wiki Mkuu wa Jeshi la Polisi , Inspekta Jenerali Saidi Mwema, alisema mkakati wa Polisi kwa sasa unaendana na kuwashirikisha wadau kama Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Barabarani (SUMATRA) na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA).
 
Mwema alitaja baadhi ya mikakati kuwa ni kutumia askari kanzu na kukamata wanaofanya makosa barabarani na kuwawajibisha askari na makamanda wa ngazi mbalimbali, wakiwemo wa mikoa, ambao wanahusika moja kwa moja na kukithiri kwa ajali katika maeneo yao.
 
Timu ya Polisi, kwa kushirikiana na wadau wengine wa usalama barabarani, ilifanya utafiti kwa miezi tisa na kupata picha halisi ya hali ya usalama barabarani, ambayo Mwema alisema inaonyesha hali ni mbaya.
 
Pia Mwema, alisema suala la usalama barabarani sasa hivi ndilo linafuatiliwa kwa karibu kutokana na kusababisha vifo na madhara mengi, baada ya kupatikana mafanikio kwa upande wa ujambazi wa kutumia silaha.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.