Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wafanyakazi vyuo vikuu kupeleka kilio kwa Rais
Wafanyakazi vyuo vikuu kupeleka kilio kwa Rais
By Habari Tanzania | Published  11/2/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Peter Orwa
 
CHAMA cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Ufundi Stadi, Habari na Utafiti (RAAWU), kimetangaza kufanya maandamano Novemba 16, mwaka huu, kwenda kumwona Rais Jakaya Kikwete, kumweleza kuhusu dhuluma ya maslahi ya wafanyakazi waendeshaji wa vyuo vikuu vya umma nchini.
 
Hatua hiyo iliafikiwa jana, katika mkutano matawi yote ya RAAWU mkoa wa Dar es Salaam, uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Chang’ombe, Dar es Salaam.
 
Katibu Mkuu wa RAAWU, Aldegunda Mgaya, alisema jana ofisini kwake kuwa chama chake kimeamua kulichukua suala hilo kuwa lake na si la vyuo vikuu tena ili kuongeza msukumo wa madai yao.
 
Mwezi uliopita, Aldegunda katika tamko alilolitoa kwenye vyombo vya habari, alisema RAAWU ingeitisha maandamano iwapo madai yao yasingeridhiwa hadi jana.
 
Madai ya watumishi waendeshaji wa vyuo vikuu yanatokana na malalamiko dhidi ya utekelezaji wa ripoti ya Tume ya Tume ya Rais iliyoundwa Septemba mwaka jana iliyoshauri waongezewe mishahara kwa asilimia 100 kwa awamu tofauti.
 
Utekelezaji ulifanyika kwa wanataaluma kama ilivyopendekezwa, na kwamba wafanyakazi waendeshaji hawakunufaika na utekelezaji wa ripoti ya Tume.
 
Kutokana na hilo, alisema Aldegunda, wawakilishi wa wafanyakazi waendeshaji walifanya jitihada za kufuatilia madai yao hadi kwenye mamlaka mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kumuona Katibu Mkuu Kiongozi na wakaishia kugonga mwamba.
 
Aldegunda hakufafanua juu ya idadi ya wanachama watakaoshiriki maandamano,wala mpangilio wa mahali yatakapoanzia na kumalizikia, akitamka tu kuwa “ni jambo litakalojulikana baadaye”.
 
Nalo Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), katika ripoti yake mkutanoni jana, lilisema litaiunga mkono RAAWU iwapo serikali haitaridhia utekelezaji wa madai yake kabla ya tarehe ya maandamano.
 
“Endapo serikali itaendelea kulipuuza suala hili, Shirikisho litaunga mkono hatua zozote zitakazochukuliwa na wafanyakazi na chama chao (RAAWU) kwa ajili ya kutetea maslahi yao,” ilisema taarifa ya TUCTA.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.