Kibondo
Chama cha msalaba mwekundu Tanzania chini ya mradi wa pamoja tunaweza uko mbioni kutoa kitabu chenye maelekezo ya ufundishaji wa watoto na vijana juu ya masuala ya ukimwi.
Meneja wa kitengo cha afya cha shirika hilo Dr. Justin Lugoi amebainisha hay oleo wakati akiongea na wawakirishi wa idara mbalimbali za halmashauri ya wilaya na wawakilishi wa madhehebu ya dini.
Dr. Lugoi amebainisha kuwa kwa pamoja wanajadili na kupitia mtaala uliomo katika mwongozo wa awali na kutoa mtaala mpya ambao utabainisha wazi mbinu za mawasiliano ya wazazi kwa watoto.
Amebainisha kuwa katika mtaala wa awali kulibainika kuwemo kwa mapungufu ambapo watoto wagodo walichukuliwa kama vijana na kupelekea kuwepo kwa ugumu katika ufundishaji wa masula ya kingono.
Amesema katika mtaala mpya unaopitiwa na wadau wa mradi pamoja na wawakilishi wengine wa mapambano dhisdi ya ukimwi masuala ya utamaduni, maadili ya mila na desturi yatazingatiwa bila kupotosha uharisia wa tatizo la UKIMWI.
Dr. Lugoi umri wa vijana utazingatiwa sana ili ujumbe wa Ukimwi upelekwe kwa uhaklika zaidi ingawa amewataka wazazi kufungua wigo wa mawasiliano baina yao na watoto ili kuvunja ukimya