HATUA kali za kisheria zitachukuliwa na serikali kwa wamachinga watakaouza viwanja kwa wenzao, ambavyo serikali imevitoa bure ili waweze kufanyia biashara.
Taarifa hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na Ofisa Habari wa Manispaa ya Ilala, Lucy Semindu.
Alisema kumezuka tabia kwa baadhi ya wamachinga, hasa kwenye maeneo ya Kibasila na Kigogo Sambusa, ambako walioshika viwanja huwauzia wenzao kwa bei ya juu kinyume cha utaratibu.
“Viwanja wamepewa bure na serikali, machinga atakayebainika anamuuzia mwenzake kiwanja ambacho yeye amepewa bure na serikali, hatua kali zitachukuliwa,” alisema Semindu.
Hivi karibuni, serikali mkoani Dar es Salaam iliwahamisha wamachinga kwenye maeneo yasiyoruhusiwa kisheria na kuwapeleka kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao