Na Mwandishi Wetu RAIS Jakaya Kikwete anaondoka leo nchini kuelekea nchi kadhaa za Asia, Falme za Kiarabu ambako atakuwa na ziara ya zaidi ya wiki mbili.
Taarifa ya Ikulu iliyotolewa jana ilieleza kuwa ziara hiyo ambayo ni kutokana n a mwaliko wa viongozi wa nchi hizo.
Ziara hiyo, ambayo ni mfululizo wa safari zake, itamfikisha Japan, China, Korea Kusini pamoja na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE). Rais atarejea nchini Novemba 13.
Katika ziara hiyo Rais Kikwete ataongoza na mkewe, Salma, Waziri wa Mipango, Uchumi, Uwezeshaji, Dk Juma Ngasongwa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Zanzibar (Fedha na Uchumi), Mwinyihaji Makame .
Wengine ni Naibu Waziri wa Fedha, Mustafa Mkullo na Mbunge wa Muhambwe, Felix Kijiko.