Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Serikali kugawa viwanja Kibada
Serikali kugawa viwanja Kibada
By Habari Tanzania | Published  10/27/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:
Na Peter Orwa
 
SERIKALI kuanzia Desemba mwaka huu, itaanza kugawa viwanja 5,000 vinavyoendelea kupimwa katika eneo la Kibada, wilayani Temeke.
 
Meneja wa Mradi wa Upimaji Viwanja 20,000 jijini Dar es Salaam, Venant Mugemuzi, aliliambia gazeti hili jana kuwa, hadi sasa vimeshapimwa viwanja 2,861 na kazi hiyo inatarajiwa kukamilika kabla ya Desemba.
 
Alisema upimaji viwanja vya Kibada, unafanywa na tatasisi tatu, mbili za serikali na moja binafsi ambazo hakuzitaja.
 
Kwa mujibu wa Mugemuzi, gharama za kulipia kiwanja itatokana na gharama iliyotumika katika kazi ya kupima, kwani ndio mtindo unaotumika katika kutoza gharama za kulipia kiwanja.
 
Wiki hii, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, ilitangaza ugawaji wa viwanja 281 eneo la Kinyerezi.
 
Hata hivyo, taarifa kutoka wizara hiyo, ilisema viwanja vya Kinyerezi vimegawiwa chini ya uratibu wa mradi wa viwanja 20, 000, ingawa havimo katika mradi wenyewe.
 
Mugemuzi alisema serikali inaendelea kugawa viwanja katika eneo la Buyuni, wilayani Ilala ambapo hado vimebakia wastani wa viwanja 2,000 kati ya 5,000 vilivyopo.
 
Alisema baadhi ya wafanyakazi wa serikali waliojiunga kupitia wizara zao kwa pamoja wamekuwa wakifika kuchukua fomu.
 
Mugemuzi alitoa mfano wa Wizara ya Mambo ya Ndani wamechukua fomu za viwanja 1,807 na Mfuko wa Akiba ya Mashirika ya Umma, imechukua fomu 500.
 
“Katika mwaka huu wa fedha, Kibada ndiyo eneo la mwisho,” alisema Mugemuzi na kuongeza kuwa baada ya hapo serikali itaelekeza nguvu zake katika mikoa ya Morogoro na Mwanza.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by kavandimwe)
    Rating
    salamu kwa wagawa viwanja hivyo viboada vya biashara ?mimi natakakiwanja cha kuishi
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.