Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Changamoto yatolewa kukabili umasikini
Changamoto yatolewa kukabili umasikini
By Habari Tanzania | Published  10/27/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Furaha Omary
 
NCHI wanachama wa Umoja wa Mataifa (UN) zimepewa changamoto ya kushirikiana kukabiliana na umasikini uliokithiri, ujinga na maradhi.
 
Hayo yalisemwa jana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Asha Rose Migiro wakati wa maadhimisho ya miaka 61 ya UN, yaliyofanyika ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam.
 
Dk. Asha Rose alisema: “Umasikini uliokithiri ndio changamoto inayokwamisha juhudi za Umoja wa Mataifa kufikia malengo yake ya Milenia ya 2015.”
 
Alisema kwa sasa duniani watu zaidi ya bilioni 1.3 wanaishi kwa matumizi ya chini ya dola moja kwa siku.
 
Mratibu Mkazi wa UN, Oscar Fernandez, alitaka maadhimisho hayo yatumike kutathmini mafanikio na pia kupanga malengo ya kimaendeleo.
 
Fernandez aliisifu Tanzania kutokana na uwezo walionao viongozi wake kiutendaji, hali inayoendelea kuiweka kuwa nchi ya amani na utulivu.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.