Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Halmashauri zenye hati chafu za hesabu zaonywa
Halmashauri zenye hati chafu za hesabu zaonywa
By Habari Tanzania | Published  05/29/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
RC Mtwara asema zinamkera na kumtia kichefuchefu
 
Aonya watendaji wasiobadilika atawafuta kazi bila huruma
 
Mhasibu halmashauri Mtwara/Mikindani Apewa miezi miwili
 

MKUU wa Mkoa wa Mtwara Henry Shekiffu amewaonya watendaji wakuu wa halmashauri zote mkoani mwake watakaoendelea kupata hati chafu za hesabu, watakosa kazi bila huruma.
 
Onyo hilo alilitoa jana wakati alipotembelea Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara, Mikindani ambapo alipata taarifa ya kazi na kuzungumza na wakuu wa idara, watumishi na madiwani ambapo alisema taarifa za hati chafu za hesabu za halmashauri zake zinamtia kichefuchefu.
 
Ametoa miezi mitatu kwa halmashauri hizo kukamilisha uandikaji wa vitabu vya hesabu na kumpa taarifa, na endapo kuna matatizo ya kukwamisha kazi hiyo apewe taarifa mapema ili hatua zinazohitajika zichukuliwe mara moja.
 
Akionyeshwa kukerwa na kwamba onyo lake siyo mzaha, mkuu huyo wa mkoa ambaye maelekezo yake hayo ya kazi yalitokana na taarifa ya kazi waliyomsomea, alimtaka Mhasibu wa Halmashauri hiyo kusafisha hesabu zake katika kipindi cha miezi miwili vinginevyo atamfukuza kazi.
 
“Yupo Mhasibu hapa, eenhe ni wewe ninakupa miezi miwili kusafisha hesabu zako za 2005, na kama bado itatolewa hati chafu fungasha virago uondoke,” alimweleza mweka hazina huyo ambaye naye alisema idara yake inakabiliwa na uhaba wa wafanyakazi wenye sifa zinazostahili.
 
Mkuu huyo wa mkoa huu ambaye huo ulikuwa mwanzo wa ziara zake za kuzitembelea halmashauri za mkoa, alisema wakurungezi ambao Mamlaka zao zitakumbwa na kuendelea kupata hati chafu wataondolewa bila msamaha wo wote.
 
“Wewe Mkurugenzi kama halmashauri yako itapata hati chafu ya hesabu ya mwaka uliyopita, basi ujuwe kibarua chako kimeota nyasi,” Shekiffu alimwonya mtendaji mkuu wa Manispaa hiyo na kuongeza kuwa hilo halina huruma wala msamaha kwa wakurugenzi wote.
 
Habari zilisema halmashauri za mkoa huo zimekuwa zikipata hati chafu kila mwaka, Manispaa ya Mtwara/Mikindani ikiwa mojawapo jambo ambalo lilimsikitisha mkuu huyo wa mkoa na kuahidi kulivalia njuga kuhakikisha mapato na matumizi ya mamlaka hizo sasa zinakuwa za uadilifu mkubwa ili kujikomboa na jinamizi la kupata hati chafu.
 
Alifafanua athari kubwa ya kupata hati chafu kuwa ni pamoja na kukosa ruzuku kubwa ya maendeleo inayotolewa na serikali kwa Halmashauri inayopata hati safi na kwamba yeye hatavumilia uzembe wa watendaji uwakosesha wananchi fursa hiyo ya kupata fedha hizo.
 
Aliwataka madiwani kusimamia kazi hizo na pia utendaji wa halmashauri zao, lakini wasibadilike na kuwa watendaji, bali zitumike sheria na kanuni katika utendaji wa kazi za kila siku na kamwe kusiachwe mwanya wa kuharibika jambo kutokana na kutotumia kanuni.
 
Hata hivyo, alisiifu halmashauri hiyo kwa kazi nzuri katika maeneo mengi kwa mujibu wa taarifa ya kazi aliyopewa, ingawa hakuridhishwa na baadhi ya maeneo na kusizitiza kuyafanyia kazi kwa maelekezo aliyotoa.
 
Kutoka gazeti la Uhuru
ISSN 0876-3896 NA.19321
Rashid Mussa, Mtwara

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.