Na Milka Ezekiel, Singida
UONGOZI wa Serikali Mkoani Singida umetoa siku saba kwa wananchi waliovamia msitu wa hifadhi wa Minyughe waondoke, vinginevyo wataondolewa kwa nguvu.
Kaimu Mkuu wa Mkoa, Florence Horombe alitoa agizo hilo mwishoni mwa wiki wakati akizungumzia amri iliyotolewa kwa wananchi hao tangu Aprili mwaka huu.
Alisema tangu Aprili mwaka huu, wananchi hao waliamriwa na Mkuu wa Mkoa, Vincent Parseko Kone kuondoka katika hifadhi hiyo, lakini wamekaidi.
Hadi sasa, kaya 641 zimehamia katika hifadhi hiyo ya Miyughe, jambo ambalo Horombe alisema ni kinyume cha sheria.
Horombe ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ta Singida, alisema kaya hizo zimepewa hadi Oktoba 27 kuwa zimeondoka katika hifadhi hiyo ambayo ni rasilmali kwa mkoa na taifa kwa jumla